Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

FCS Narrative Report

Introduction

Tanzania Women Social Economic Development and Human Rights Organization
kama ilivyo hapo juu
Kuongeza uelewa, Utetezi na ushawishi katika utekelezaji wa Sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia ya mwaka 2000 ili kuongeza mapambano dhidi ya vitendo vya kinyama wafanyiwavyo wanawake katika wilaya za Kasulu na Kigoma (Vijijini).
FCS/MG/1/10/204
Dates: Januari 25-Aprili 25, 2011Quarter(s): Robo ya kwanza 2011
William Daudi
TWSEDHRO
S.L.P 579
Kigoma Tanzania

Project Description

Policy Engagement
Kwanza kabisa mradi unakidhi malengo katika eneo hili la sera kwa kuwa mradi ulilenga/unalenga kusimamia utekelezaji wa Sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia ya mwaka 2000 ili kuongeza uelewa katika ngazi ya Wilaya kwa kutoa mifano hai ya unyanyasaji wa jinsia waliopitia wanawake mbalimbali na namna ambavyo bado jamii nyingi hasa vijijini zinavyoendelea kumnyima haki mwanamke katika nyanja mbalimbali kutokana tu na jinsia yake na si uwezo wake wa kiutendaji. Mradi umekidhi lengo la sera kwa kuwa mradi umetoa fursa kwa wanawake walionyanyasika kupitia hali ngumu kutoa uzoefu mbele ya majukwaa ya ushawishi na mifano hiyo kuwa chachu ya kutengeneza /kuweka mikakati ngazi ya wilaya kupambana na hali hiyo. Aidha mradi umekidhi haja kwa kuwa ufafanuzi juu ya sera na wajibu wa viongozi wa kata, wawakilishi wa wananchi na viongozi wa dini na asasi walijengewa uwezo wa uelewa wa sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia ya mwaka 2000.
RegionDistrictWardVillagesTotal Beneficiaries
KigomaKigoma (Vijijini)Kagongo30
Mukigo30
Nguruka30
KasuluKasulu Mjini40
Kasangezi48
Nyakitonto47
 Direct BeneficiariesIndirect Beneficiaries
Female7936,800
Male14631,200
Total22598,000

Project Outputs and Activities

- Vipeperushi vilivyotafsiriwa kwa lugha rahisi vimeandaliwa na kusambazwa ili wananchi wengi zaidi waifahamu sera.

- Mikutano ya utetezi na ushawishi ngazi ya Kata/Wilaya imefanyika na mikakati juu ya ufuatiliaji wake imeandaliwa.
-

1. Kuandaa mikutano sita katika ngazi ya Kata kwa kila Kata yenye lengo la kuwakutanisha wajumbe wa mabaraza ya Kata na wawakilishi wa wananchi ili kutoa ufafanuzi juu ya sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia na pia kueleza nafasi yao katika kutekeleza sera hiyo. ( siku mbili kwa kila kata)

2. Kutengeneza vipeperushi na mabngo ( Posters) yenye tafsiri rahisi ya sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia na kuvisambaza kwa wingi katika maeneo ya vijijini ili wananchi waweze kuielewa sera na kufuatilia utekelezaji wake.
3. Kuunda vikosi vya ufuatiliaji wa masuala ya unyanyasaji wa wanawake vijijini ( Gender Violance Monitoring Group) na kuripoti na pia kutafuta mfumo bora wa kuripoti matukio hayo.
4. Kuendesha mikutano majukwaa ya utetezi na ushawishi ambapo wahanga wa matukio ya unyanyasaji wataalikwa kutoa changamoto walizopitia na mikakati ya pamoja kuandaliwa.
Kamati ya mradi kwa kushirikiana na wadau ilifanikiwa kutekeleza haya yafuatayo;
- Kuandaa vipeperushi 2,000 na mabango 1,000(Posters) na kuyasambaza katika kata zote sita yaani: Kagongo, Mukigo, Nguruka, Kasulu Mjini, Kasangezi/Kigembe, na Nyakitonto.

- Kuendesha mikutano sita katika kata sita ambapo mkutano uliendeshwa kwa muda wa siku mbili kama ilivyo pangwa kwa kila kata, jumla ya washiriki 30 walihudhulia kwa kila kata ambapo kwa ujumla jumla ya washiriki 180 walihudhulia mkutano huo.
Mkutano huo wa ufafanuzi wa sera na wajibu wa viongozi katika kutekeleza sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia ya mwaka 2000, ulitekelezwa katika kata sita ambazo ni: kwa Kigoma Vijijini):- Kagongo, Mukigo, na Nguruka. Kwa Kasulu ni: Kata za kasulu Mjini, Kigembe/Kasangezi na Nyakitonto.

Masuala yaliyoshughulikiwa ni pamoja na haya yafuatayo;
- Ufafanuzi kuhusu Sera ya Maendeleo ya wanawake na jinsia ya mwaka 2000
- Wajibu wa Viongozi katika kutekeleza Sera ya maendeleo ya wanawake na Jinsia ya mwaka
2000.
- Hali ya vyombo vya kusimamia, kutekeleza na kutoa haki kwa wanawake katika kata husika.
( hii ilikuwa ni kwa siku ya Kwanza)

Siku ya Pili:- tulishughulikia haya:
- Ushiriki wa jamii haswa wanaume na wanawake katika shughuli za kiuchumi/maendeleo.
- Aidha tulifanya majadiliano kuhusu changamoto juu ya wajibu wa viongozi katika kutekeleza sera ya MWJ ya mwaka 2000 na nini kifanyike ili kukabiliana na changamoto hizo.

Wapi:- katika kata sita za mradi kama ilivyotajwa huko nyuma. Maswala haya yaliwahusu viongozi wa mabaraza ya Kata na wawakilishi wa wananchi katika kata sita za mradi.

Idadi kwa kila kata ilikuwa washiriki 30, ambapo jumla ya washiriki 180 walinufaika na mafunzo hayo.

Mafanikio ya jumla.
1. ushirikiano mzuri kati ya watendaji wa Kata na shirika letu na hatimaye kufanikiwa kufanyika kwa mikutano yote 12( kwa kata sita kila Kata siku mbili) kama ilivyopangwa.
2. kupokelewa vizuri kwa sera na kueleweka miongoni mwa viongozi washiriki wa mikutano hiyo.
3.Viongozi kutambua changamoto zinazowakabili na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo.
4. Ujembe wa sera kuwafikia/kuifikia jamii kwa urahisi kupitia vipeperushi na mabango yenye ujumbe murua/mwepesi.
6. jamii kutambua haki zao za msingi kama Sera inavyofafanua.
7. Kuanza kuripotiwa kwa matukio ya unyanyasaji kijinsia kupitia ofisi zetu za kigoma na Kasulu.
8. Shirika letu ikiwa ni pamoja na FCS kuendelea kufahamika miongoni mwa jamii haswa ngazi ya vijiji na Wilaya.
9. Ushiriki wa vyombo vya habari katika shughuli zetu kama vile: ITV, RFA, Radio Kwizera, Star TV, channel Ten, na vyombo vya magazeti kama Uhuru, Habari leo n.k.
10. Shirika kufanikiwa kupata usafiri wa Pikipiki, pamoja na vitendea kazi kama vile Scanner machine na mtando wa internet na Printer.

Kwa kifupi hakuna tofauti yoyote iliyojitokeza na kufanya mafanikio au matokeo ya awali kuwa tofauti. badala yake tunaona mafanikio makubwa tofauti na tulivyofikiria awali.
Katika kutekeleza mradi wetu. rasilimali zilizotumika ni rasilimali fedha kama ifuatavyo:-
Shuguli ya Kwanza: Kuandaa mikutano sita katika ngazi ya kata kwa kila kata yenye lengo la kuwakutanisha wajumbe wa mabaraza ya kata na wawakilishi wa wananchi ili kutoa ufafanuzi juu ya sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia na pia kueleza nafasi yao katika kutekeleza sera hiyo. (Siku mbili kila Kata)
1. Chakula kwa washiriki 30@ 5000 x 30 x 2 x kata 6 = 1,800,000
2. soda/maji kwa washiriki 30@1000 x 30 x siku 2 x Kata 6 = 720,000
3. Chai washiriki 30@ 1000 x 30 x 2 x kata 6= 360,000
4. Ununuzi wa limu kwa ajili barua za mialiko limu 4@ 10,000 x 4= 40,000
5. Ununuzi wa Bahasha 190@50x 190= 9,500
6. Note Book 180@1000 x 180= 180,000
7. Flip chart 5@ 8000 x 5= 40,000
8. marker Pen Box 5@ 7000x 5= 35,000
9.Maskin Tape 15@500 x 15= 7500
10.nauli kwa wawezeshaji na watendaji wa asasi @ 15000 x 3 x 2 x6 540,000
11. Ukumbi 100000 x 2 x Kata 1(Kasulu mjini) 200,000
12. Gharama za wawezeshaji 50000 x wawezeshaji 2 x 2x siku 12= 1,200,000
13. Malazi na chakula cha usiku kwa wawezeshaji 2+ Mratibu 540,000
Jumla kwa shughuli ya kwanza (zilizotumika) ni 5,672,000


2. shughuli ya Pili: Kutengeneza vipeperushi na mabango yenye tafsiri rahisi ya sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia na kivisambaza kwa wingi katika maeneo ya vijijini ili wananchi waweze kuielewa sera na kufuatilia utekelezaji wake.

1.2.1 Kutengeneza vipeperushi 2000@ 1000 x 2000 2,000,000
1.2.2 kutengeneza Mabango Posters 1000@ 1000 x 1000 1,000,000
1.2.3 Gharama za usambazaji kwa kata 6.@ 10,000x6 60,000
Jumla ya ndogo (Matumizi) 3,060,000


3. Shughuli ya Tatu: Kuendesha Mikutano /Jukwaa la utetezi na ushawishi ambapo wahanga wa matukio ya unyanyasaji walialikwa kutoa changamoto walizopitia na mikakati kuandaliwa.
( Wilaya ya Kasulu). mkutano/Jukwaa mmoja ( robo ya kwanza)

3.1. Gharama za ukumbi kwa siku 1@ 100,000 x 1 100,000
3.2. Gharama za mwezeshaji 1@ 100,000 x siku moja 100,000
3.3. Gharama za chai washiriki 50 @2000 x 50 x siku moja 100,000
3.4. Chakula cha mchana kwa washiriki 50 @ 5000 x 50 x 1 250,000
3.5. Malazi washiriki (toka Vijijini 40 @10,000 x 40 x 1 400,000
3.6. Usafiri wa wawakilishi toka vijijini 40@ 15,000 x 40 x siku 1 600,000
3.7. Note Book kwa washiriki 50@ 1000 x 50 50,000
3.8. Chakula cha usiku kwa washiriki 40 toka vijijini @ 5000 x 40 x 1. 200,000
Jumla ya Matumizi (kwa Wilaya ya Kasulu) 1,800,000


4. shughuli ya Nne: Ufuatiliaji na Tathimini Ufuatiliaji kufanyika angalau mara moja kwa mwezi ili kuona jinsi watendaji wa kata wanavyotekeleza Sera katika kata husika.

4.1. Ununuzi wa Petrol ya Pikipiki ( Ufuatiliaji) lita 61.25 @ 2000 x 61.25 122,500
4.2. Ununuzi wa limu A4 kwa ajili ya fomu za tathimini. @ 10,000 x 4 38,000
4.3. Chakula na malazi siku 2 kila kata @15000 x siku 2 x kata 3 90,000
4.4. Mwezeshaji wa tathimini siku 3 kwa kata 3@ 100,000 x3 300,000
4.5. Nauli watendaji 3@ 10,000 x 4 x siku 3 120,000
4.6. Chakula na malazi wakati wa tathimini watu 4@ 15,000x 4 x 3 180,000
Jumla ya matumizi sughuli ya nne: 978,000

Gharama za utawala.

6.1. Posho ya mratibu miezi mitatu @200,000 x 3 = 600,000
6.2. Posho ya Mhasibu/Mtunza Hazina Miezi Mitatu @ 150,000 x 3= 450,000
6.3. Gharama za mawasiliano kila mwezi Miezi 3@ 20,000 x 3 60,000
6.4. Ghaarama za shajala kwa mwezi @20,000 x 3 60,000
6.5. Gharama za pango (Ofisi) kwa Mwezi @50,000 x 3 150,000
6.6. Ununuzi wa pikipiki 1@ 2,450,000 2,450,000
6.7. Ununuzi wa Printer 1@ 500,000 x 1= 500,000
6.8. Kuweka Internet ( Zain Mordem) 1 @ 100,000 100,000
6.9. Ununuzi wa wino wa printer 1 Catridge Hp 12A @ 60,000 165,000
6.10. Ununuzi wa scaner Machine 1@330,000 x 1 330,000
Jumla ya gharama za matumizi Utawala 4,865,000



Project Outcomes and Impact

- Uelewa wa sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia umeongezeka miongoni mwa viongozi wa serikali za mitaa na wawakilishi wa wananchi na wanashiriki kikamilifu kutekeleza na kupambana na vitendo vya unyanyasaji kijinsia dhidi ya wanawake katika halmashauri za Kigoma na kasulu.

- Matukio mbalimbali ya unyanyasaji kijinsia dhidi ya wanawake yameripotiwa na hatu zinachukuliwa kwa wahusika kama sehemu ya mikakati ya mabaraza ya kata na Halmsahuri za Wilaya husika kupambana na tatizo hilo.
- Mabaraza ya kata yamejiongezea uelewa na kwa sasa wametambu wajibu wao katika kutekeleza sera kwa vitendo katika kata zao.
- Wanawake kuwa na ujasiri katika kueleza changamoto walizokutana nazo dhidi ya vitendo vya unyanyasaji kjinsia.
-Wanawake wametambua wapi wapeleke kesi zao dhidi ya vitendo vya unyanyasaji kijinsia na sasa wameanza kuripoti vitendo wanavyotendewa vya unyanyasaji.
- Kuwekwa kwa mpango maalumu wa kuiomba serikali utunge sheriaitakayotoa adhabu kali kwa wanaume na wanawake wanaotekeleza familia zao. ( Mapendekezo ya wadau wa mradi)
Mabadiliko mengine ni:-
- Baadhi ya Serikali za Vijiji zilikuwa haziendeshi mikutano ya robo mwaka, sasa wameanza katika Kata ya Kagongo.
- Uongozi wa Kituo cha afya Nguruka, umetambua umhimu wa utekelezaji wa sera kwa vitendo na sasa unahamasisha jamii kupanga uzazi na kutambua umhimu wa wanawake wajawazito kuhudhulia kliniki.
-Vyombo vya habari sasa vimeanza kualika watendaji wa asasi yetu katika mijadala ya moja kwa moja katika studio zao zilizoko kigoma na kushiriki kutoa elimu kwa njia ya radio, Kama vile kipindi cha darubini, na Asubuhi njema. ( RFA na radio kwizera) haya ni mabadiriko makubwa.
- Ubora wa mada zilizowasilishwa na wawezeshaji wetu.
-Ubora wa lengo mahsusi la mradi.
-mabango yalibandikwa katika maeneo mbalimbali yameongeza uelewa zaidi hata kwa wale ambao hawakushiriki moja kwa moja kwa mradi.
-Jinsi asasi yetu ilivyowashirikisha waandishi wa habari katika mradi wetu.

Lessons Learned

Explanation
Katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo wa mradi huu, tumepata mawazo makuu mapya yafuatayo kama sehemu ya uzoefu:
1. Sera nyingi zinazoandaliwa na serikali hazifiki/kuwafikia wadau wa maendeleo haswa ngazi ya Kata na Vijiji.
2. Katika kutekeleza mradi huu, tumejifunza kuwa ndoa nyingi ziko katika mazingira magumu kutokana na hali ya mfume dume kuendelea kushamiri katika maeneo yote ya tulikotekeleza mradi huu.
3.Viongozi wengi wa mabaraza ya Kata hawajui wajibu wao.
Mabaraza ya Kata yaliyo mengi yanaendesha shughuli za utoaji haki kwa uzoefu na hayana mwongozo wa sheria mbalimbali.
Ipo haja ya asasi za kirai kusaidia kuwajengea uwezo jamii haswa wale walioko katika famili kufundishwa juu ya kuwa na maadili mema, haswa katika kipindi cha malezi ya mtoto ili kuwa na taifa lenye viongozi na jamii bora siku zijazo.
Tumejifunza kuwa vyombo vya habari ni mhimu sana katika kushirikishwa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali na hivyo itasaidia jamii kubwa zaidi kushiriki katika mijadala kwa njia ya radio, hatimaye jamii itakuwa na mabadiliko makubwa kijamii, kielimu, kiutamaduni na kiuchumi.
Utegemezi wa vyombo vya usafiri kwa asasi za kiraia unaweza kuchangia kuchelewa kufikia malengo waliyojipangia.
Mfumo wa mahusiano ya viongozi wa vyama vya siasa ngazi ya Kata hadi Vijiji unachangia kuzorotesha masuala ya utekelezaji wa sera haswa ya maendeleoa ya wanawake na jinsia. hivyo tumejifunza kwamba ipo haja ya asasi za kiraia kutoa elimu kwa viongozi wa vyama vya siasa toka ngazi ya Wilaya hadi Kijiji ili watambue umhimu wa siasa katika kutekeleza sera mbalimbali za Serikali.

Challenges

ChallengeHow it was overcome
Kwa ujumla hakuna changamoto zilizojitokeza na kusababisha kutofikia malengo. hata hivyo changamoto kubwa ilikuwa kwenye bajeti yetu haswa kwenye upande wa nauli za washiriki wa mkutano ngazi ya Kata. Kwenye bajeti tulijikuta kifungu cha nauli hakiupo. Tulifanya majadiliano na Watendaji wa Kata ili waweze kutusaidia kutumia Madarasa ya Shule za Msingi/Sekondari bila gharama ili gharama za kulipia ukumbi zitumike kulipia nauli. Isipokuwa kwa upande wa kasulu tulipunguza gharama ya matumizi ya ununuzi wa petroli na kulipia ukumbi.

Malalamiko ya washiriki juu ya kiwango cha nauli kilicholipwa cha Tsh 5000, wakati wa mikutano ya Kata kuwa kidogo.

Linkages

StakeholderHow you worked with them
Serikali za Mitaa:
- Watendaji wa Kata
Kabla ya mradi kufanyika, shirika letu lilifanya mawasiliano na Watendaji wa kata kwa kupeleka barua za utambulisho wa mradi, katika barua hizo, tulieleza lengo la mradi, kiasi cha fedha kilichotolewa na FCS, aina na idadi ya walengwa wa mradi. Aidha Uongozi wa shirika letu, Watendaji wa Kata, kwa kusirikiana na watendaji wa Vijiji tulifanikiwa kuwapata washiriki wa mikutano ya mabaraza ya Kata na washiriki wa jukwaa la utetezi na Ushawishi juu ya haki za wanawake na jinsia.
Vyombo vya habari
-Radio Kwizera-Kigoma
-Radio Free Africa
- Star TV
-ITV
-Magazeti Uhuru, Jambo leo.
Vyombo hivi vya habari, tulivishirikisha ili wahusika ( waandishi wa habari) nao wachangie hoja katika mijadala, kutokana na uzoefu walionao. aidha lengo lingine la kuwashirikisha ilikuwa kusaidia kufikisha ujumbe kwa jamii ( kwa kiwango kikubwa).

Kupitia vyombo, hiv
Dini.
Roman Katoliki
-FPCT
Anglican
-Islamu
Hawa walishirikishwa ili kusaidia kuleta ufanisi wa kutekelezwa kwa sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia.

Pia wao wanasikilizwa na watu wengi kulingana na hadhi yao.

Walishiriki katika shughuli zote za utekelezaji wa mradi huu kwa robo hii ya kwanza.
Vyama vya siasa.
CCM
CHADEMA
CUF
NCCR
Viongozi wa vyama walishirikishwa kwa kuhudhulia mikutano ya Mabaraza ya Kata. na kuruhusiwa kuchangia mada mbalimbali.Lakini tuliwashirikisha ili waweze kupata ujumbe wa sera, kwani wanawake wengi wanapojitokeza kugombea nafasi za uongozi (Kisiasa) baadhi ya viongozi wa vyama huwakwamisha wanawake katika kiny'nganyiro cha kura za maoni. na hivyo kufanya sera hii isitekelezeke.
Idara ya Afya:
Mabwana Afya
Wakuu wa vituoa vya afya.Zahanati
hawa tuliwashirikisha ili waweze kuitambua sera kwa kuhdudhuria mikutano ya Kata, iliyoendeshwa kwa muda wa siku mbili kila kata. lengo lilikuwa ni kuwawezesha kuijua sera na kisha kuitekeleza kwa vitendo kwa kutoa huduma bora kwa Haswa mama wajawazito na watoto.

Future Plans

Activities Planned1st Month2nd Month3rd Month
Kuunda Kikosi cha wafuatiliaji wa masuala ya unyanyasaji wa wanawake vijijini ( Gender Violance Monitoring Group) na kuripoti na pia kutafuta mfumo bora wa kuripoti matukio hayoxxxx
kuendesha jukwaa la utetezi na ushawishi ambapo wahanga wa matukio ya unyanyasaji wataalikwa kutoa changamoto walizopitia na mikakati ya pamoja kuandaliwa.xxxx
Kufanya ufuataliaji na tahimini kwa kutemebelea Kila kata angalau mara moja kwa mwezixxxxxx
gharama za utawala: Posho,Mawasiliano na shajala.xxxxxxxxx

Beneficiaries Reached

    Direct BeneficiariesIndirect Beneficiaries
WidowsFemale(No Response)(No Response)
Male(No Response)(No Response)
Total(No Response)(No Response)
People living with HIV/AIDSFemale(No Response)(No Response)
Male(No Response)(No Response)
Total(No Response)(No Response)
ElderlyFemale(No Response)(No Response)
Male(No Response)(No Response)
Total(No Response)(No Response)
OrphansFemale(No Response)(No Response)
Male(No Response)(No Response)
Total(No Response)(No Response)
ChildrenFemale(No Response)(No Response)
Male(No Response)(No Response)
Total(No Response)(No Response)
DisabledFemale(No Response)(No Response)
Male(No Response)(No Response)
Total(No Response)(No Response)
YouthFemale(No Response)(No Response)
Male(No Response)(No Response)
Total(No Response)(No Response)
OtherFemale7931200
Male14636800
Total22568000
(No Response)

Events Attended

Type of EventWhenLessonsActions Taken
mafunzo ya usimamizi wa ruzukuAgosti Umuhimu/Usimamizi wa fedha
- udhibiti wa fedha
- Utenganishi wa majukumu
Madaraka na mipaka yake
- Uandaaji na uhifadhi wa kumbukumbu za mahesabu
- Uandaaji w taarifa ya fedha-foundation.
kutekeleza mafunzo hayo kwa vitendo, kwa kuandaa vitabu vya kumbukumbu za fedha, na nyaraka nyingine kama voucher, fomu ya kuombea fedha, na mikataba ya wawezeshaji .
kuweka kumbukumbu vizuri
Uandishi wa taarifakufuata hadidu za rejea za somo hili na kuzitekeleza kwa vitendo wakati wa uandishi wa taarifa zetu za shirika.

Attachments

« Previous

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.