Asili (Kiswahili) | Kiswahili |
---|---|
Katika majumuisho ya wiki hii,tumugundua sababu kubwa zinazosababisha migogoro isiyoisha inayoikumba serikali yetu ya Tanzania.Hii ni kutokana na tabia za watanzania ambao wamezoea kulalamika bila kuchukua hatua,vile vile watanzania tuna kasumba ya kusahau.Kutokana na sababu hizi watanzania tuamke ,tuwajibike ,kwa kuchukua hatua kwa kufika mahali husika ,tupeleke ujumbe na hoja zetu kwa maandishi ili malalamiko yetu yawe na kumbukumbu ,kwani haki haipatikani bila kuipigania na hatima ya maisha yetu yapo mikononi mwetu wenyewe . Wito wetu kwa asasi za kijamii ni kuwaomba tuwajibike kwa pamoja ili kuelimisha jamii {kuijengea uwezo jamii} kuanzia ngazi ya famili , mtaa n.k ili tuunde nguvu ya pamoja itakayoondoa mifumo mibovu ya uongoziwa wa nchi yetu ambayo insababisha matatizo yasiyo kwisha kwa kila sekta ,mfano elimu ,afya. na nyingine nyingi.Kwa kuwajengea uwezo wananchi watadhibiti siasa katika sehemu za utendakazi. |
(Bila tafsiri) |
Ili kuhariri tafsiri, lazima ufungue. Fungua · Jiandikishe