Envaya

/mpalanocdo/post/14: English: WIG9VHfPPwxCkB6tDXfPViMr:content

Base (English) English

UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

La Mgambo limelia…

Kesho Jumamosi tarehe Novemba 22, saa mbili mpaka saa tatu asubihi, siku moja kabla ya kuanza zoezi la kuandikisha orodha ya wapiga kura,  Mratibu wa Asasi ya Mpalano CDO, ataruka live katika kipindi cha TUWEKANE SAWA Cha redio ya Ushindi FM 98.6 ya mjini Mbeya, kufafanua masuala mbali mbali kuhusiana na uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Desemba 14, mwaka huu.

Usikose fursa hii adhimu ili kujijengea uelewa wa masuala mbali mbali yanayohusu uchaguzi huu ikiwa ni pamoja na Uandikishaji kwenye orodha ya wapiga kura, kuhakiki majina na hatua za kuchukua ikiwa jina lako halipo ama limekaa sivyo ndivyo; uteuzi wa wagombea, kuweka pingamizi dhidi ya mgombea, kampeni na utaratibu wa upigaji kura.

Wote mnakaribishwa.

Bonyeza HAPA kusikiliza tangazo la hamasa

(Not translated)

In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register