Envaya

/jeanmedia/post/10896: English: WI000A5A0408418000010896:content

Base (Swahili) English

Mpango wa utoaji wa elimu ya watu wazima vijijini uungwe mkono

Na ASIA KILAMBWANDA

Taaluma ni nyenzo kubwa ya kufikia maendeleo , pia huharakisha mipango ya kufika katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi, kijamii na hata kisiasa bila kujali taaluma hiyo ni nadharia ama vitendo inategemea jinsi ya matumizi ya taaluma hiyo.

Katika kulifahamu hili Halmashauri ya wilaya ya Mtwara Vijijini kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la kuwahudumia watoto (Unicef), imeandaa mpango wa utoaji wa elimu kwa watoto waliopita muda wa kuandikishwa kujiunga na elimu ya shule ya msingi, elimu ya watu wazima ujulikanao kama MENKWA .

Mpango huo umetoa mafunzo ya walimu watakaoshiriki kakika ufundishaji wa wanafunzi watakaosoma elimu ya watu wazima(MENKWA),katika mkakati wa kuondoa ujinga na umasikini na kuongeza idadi ya watu wanaojua kusoma na kuandika .

Mafunzo haya yaliwashirikisha 60 na wadau wa elimu katika ngazi ya kata ili kukidhi mahitaji ya wananchi na watoto katika utoaji wa elimu husika bila kuathiri kundi au nafasi na haki ya kupata elimu.

Baadhi ya kata zilizoshiriki ni Naumbu, madimba, Tangazo, nanyamba, likomnde, Dihimba, Msimbati, Nitekela, Mgau na Malanje. Na nyingine ni mayembe chini, mchanja, msanga mkuu, chawi, libobe, Bandari, kilambo na Nachenjele.

Matarajio ya elimu au taaluma yeyote katika jamii ni kuona kwamba inaleta tija na mabadiliko katika nchi, kwa mtu binafsi na taifa kwa ujumla.

Kwa hali hii mpango wa kutokomeza ujinga hasa katika maeneo yaliyosahaulika(Vijijini) utaondoa ufinyu wa kufikiri unaowafanya vijana wengi washindwe kujituma kutokana na ukosefu wa elimu jambo ambalo ni hatari kwa maisha ya vijana.

Plan for the provision of adult education in rural areas uungwe hand

And Asia KILAMBWANDA

Professionalism is a great tool to achieve development, it also plans to speed up various aspects of economic, social and even political career regardless of it is theoretical or practical depends on how the use of that profession.

In understand this District Council Mtwara Rural in conjunction with an international organization to serve children (Unicef), has developed a program of education for children who passed the time of registration to join the education of primary school, adult education known as MENKWA.

The program has offered training to teachers who participated kakika teaching students who studied adult education (MENKWA), the strategy of removing ignorance and poverty and increase the number of people who know how to read and write.

This training yaliwashirikisha 60 and stakeholders of education in the county level to meet the needs of citizens and children in the provision of relevant education without affecting the group or place and the right to education.

Some of the participating county is Naumbu, madimba, Announcement, nanyamba, likomnde, Dihimba, Msimbati, Nitekela, Mgau and Malanje. Another is razor blades and under, immunize, Sanga general, Nawi, libobe, port, dam and Nachenjele.

Expectations of education or any profession in the community is seeing that brings productivity and changes in the country, the individual and the nation as a whole.

For this program to eradicate illiteracy, particularly in disadvantaged areas (rural) will remove the constraints of thinking you can not force commitment of young people due to lack of knowledge which is dangerous to the lives of youth.


In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register

Translation History

Google Translate
April 2, 2011
Plan for the provision of adult education in rural areas uungwe hand – And Asia KILAMBWANDA – Professionalism is a great tool to achieve development, it also plans to speed up various aspects of economic, social and even political career regardless of it is theoretical or practical depends on how the use of that profession. – In understand this District Council Mtwara Rural in conjunction with an international organization to...