Base (Swahili) | English |
---|---|
Vijana wa Africa Upendo Group wamekuwa wakikutana mara kwa mara kujadiliana maswala mbalimbali yanayohusu vijana. kutokana na wimbi la vijana wengi ambao wanamaliza vyuo vikuu lakini kutokana na mashirika na serikali kung'ang'ania kuwa vijana hawa wawe na uzoefu katika kazi na kwa kuzingatia kuwa vijana hawa ndio kwanza wanatoka kwenye vyuo wamekuwa katika kuhangaika sana. Katika asasi yetu ya Africa Upendo Group tumekuwa na kitengo maalum cha kuwasaidia vijana kama hawa kwa kuwapatia mafunzo mbalimbali na kwa pamoja kwa njia ya kujitolea tumeweza kuwa na mikutano ya mara kwa mara.Ili kubaini njia mbadala katika kuona kuwa vijana wanapokuwa bado wapo mashuleni na baada ya kutoka wanaweza kujiajiri wenyewe kwa kufanya mambo mbalimbali yakiwemo tafiti mbalimbali.Katika kuliona hili vijana hawa wametengeneza tovuti ambayo itajulikana kama www.ICT4TD.co.tz ambayo itakuwa na shughuli mbalimbali zikiwemo vijana wengi kujitolea kufundisha masomo mbalimbali kama lugha ya kijerumani,kifaransa,Kiingereza,masomo ya Teknohama watakuwa wanajitolea zaidi katika maswala yanayohusu jamii kama usafi na utunzaji wa mazingira,Makazi au kaya,vijana walioathiriwa au wako katika hatari ya kuambukizwa UKIMWI na madawa ya kulevya n.k kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo Envaya,DTBI,Restless,Global Exchange,VSO wizara ya habari utamaduni na maendeleo ya vijana . Katika kutekeleza majukumu yao mbalimbali vijana wamekuwa na makongamano mbalimbali kama siku ya kujitolea duniani ambapo vijana waliweza kubadilishana uzoefu na mambo mbalimbali pia waliweza kuhudhuria mkutano ambao ulihudumiwa wa DTBI,na kwa pamoja walikutana na vijana kutoka chuo kikuu cha MIT kutoka Marekani na kubadilishana mawazo na wamekuwa wakifanya mambo mbalimbali ya mifano ya hayo. Pia wameunda Stearing commitee ambayo itakuwa na majukumu mbalimbali kwa makundi mbalimbali.Ili kuboresha zaidi na kuhakikisha kuwa vijana wanapata taarifa za msingi kutoka nje na ndani ya nchi yao.Website hii imemalizika na iko katika hatua ya kuzinduliwa karibuni. Hapa chini utaona moja ya kamati ambayo inashughulika na kuratibu makundi mbalimbali chini ya mwenyekiti wake Albert.Huyu ni kijana aliyemaliza mafunzo ya Teknohama kwenye chuo kikuu cha Dodoma na Moderator akiwa ni Neatness Msemo ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji katika Asasi hii.
kwa kukuona picha nyingi zaidi bonyeza link hapo chini: |
Love Africa Youth Group have been meeting regularly to discuss various issues pertaining to youth. due to a wave of young people who graduated from universities but from government organizations to hold that the young people have experience in working with young people to consider that these are the first members from the colleges have been in a very distressed. In our organization of African Love Group we have a Special Unit to help young people like these by providing training and together with a commitment we can have meetings from time to mara.Ili identify alternatives to see that young people while they're still in school and after from self employment they can to make things different studies including mbalimbali.Katika see this lads have developed a website which will be determined as www.ICT4TD.co.tz which will have various activities including many young volunteers to teach various subjects like languages German, French, English , studies of ICT will be offered more in social issues such as hygiene and environmental protection, housing or households, young people affected or are at risk of contracting AIDS and drug addiction etc. in collaboration with various institutions including Envaya, DTBI, restless, Global Exchange , VSO's ministry of information culture and youth development. In order to undertake their various youth have been and conferences such as the volunteer world where young people can share experiences and different things also were able to attend the meeting which was attended to DTBI, and together they met with youth from the University of MIT from the U.S. to exchange ideas and have been worked a variety of examples of these. They have also created Stearing Committee which will have different roles in groups mbalimbali.Ili further improvement and ensure that young people receive basic information from the outside and inside the country this yao.Website been completed and are in the process of launching soon. Below you will find one of the coordinating committee that deals with various groups under the chairmanship Albert.Huyu a young man who completed training in ICT at the University of Dodoma and Neatness expression as a Moderator, who is Executive Chairman of this organization. to see you many more pictures click link below: |
Translation History
|