Fungua

/CMT/post/121812: Kiswahili: WIkrVPJbMhcRoJ4JTF6UEWy2:content

« Iliyotangulia   ·   Ifuatayo »
Asili (Kiswahili) Kiswahili

CHAMA CHA MICHEZO CHA VIZIWI TANGA

                                   (CHAMIVITA)

TANGA ASSOCIATION OF SPORTS  FOR THE DEAF (T.A.S.D)

        S.L.P 5106-TANGATANZANIA,EMAIL: deafssports@yahoo.com

                       

Kumb no. CMVT/TNG/VOL ,12/12                                                       03/05/2012

 

 KWA WADAU WOTE WA WA MICHEZO

 POPOTE TANZANIA.

KK

AFISA UTAMADUNI,

HALMASHURI YA JIJI LA TANGA,

S.L.P 178

TANGA

 Ndugu,

YAH: OMBI LA MSAADA WA  NAULI KWA AJILI YA KUSHIRIKI TAMASHA LA MICHEZO ZANZIBAR.

Somo la hapo juu lahusika sana.

 

Chama cha michezo cha viziwi Tanga-(CHAMIVITA) kinaandika barua hii kwako kwa ajili ya kupatiwa msaada wa Nauli kwa ajili ya kutuwezesha kushiriki TAMASHA LA MICHEZO KWA VIZIWI litakalofanyika Zanzibar mwezi july 23 hadi 6 Agost 2012  mwaka huu.

 

Kwa  sasa CHAMIVITA kipo katika kutafuta na kukuza ARI ya michezo kwa walemavu viziwi wa mkoa wa Tanga, kwa mujibu wa waandaaji wa TAMASHA hilo kwa CHAMIVITA TANGA tunatakiwa kujigharamia kwa mahitaji ya nauli ya kwenda na kurudi Tanga,usafiri wa ndani ya Zanzibar.kwa wachezaji 20 na viongozi 3 Aidha chakula na malazi vitatolewa na wandaaji/wenyeji ZFA na CHAMIVIZA(CHAMA CHA MICHEZO CHA VIZIWI ZANZIBAR) Mahitaji yetu ni kama ifuatavyo:-

(i)                  Usafiri wa Tanga to Dar es salaam watu 23@11,000x2x23=   Tsh     506,000.00

(ii)                Usafiri wa dar  es salaam to Zanzibar watu 23@20,000x2x23 =Tsh   920,000.00

(iii)              Usafiri wa ndani ya Zanzibar   kwa wiki mbili                             =Tsh 300,000.00  

(iv)                Dharura na matibabu                                                                   =Tsh  200,000;00

                                                       JUMLA                                                          1,926.000,00

 

Kwa mahitaji hayo hapo juu tunaomba muangalie ni jinsi gani mnaweza kutusaidia kadri ya uwezo wako ili tuweze kufanikisha Azma yetu ya kuendeleza michezo kwa walemavu viziwi wa mkoa wa Tanga.

 

Tunatanguliza shukrani za dhati kwako.

 

Wasaalam,

 

 

________________

ALLY NASSORO 

KATIBU MKUU     SIMU +225713 733 114  TUMA SMS TU.

 

________________________________________________________________________

N.B: Endapo msaada wenu utakuwa katika hundi iandikwe: JUMUIYA YA MICHEZO YA VIZIWI TANZANIA A/C NO 41 72 50 87 86 NATIONAL MICROFINANCE BANK(NMB) MADARAKA BRANCH TANGA

(Bila tafsiri)

Ili kuhariri tafsiri, lazima ufungue. Fungua · Jiandikishe