Base (Swahili) | English |
---|---|
Wananchi watakiwa kutunza mazingira Na ASIA KILAMBWANDA, Mtwara Wananchi Mkoani Mtwara wametakiwa kutotupa taka hovyo hususani katika maeneo ya pwani ya bahari ya bandari ya Mtwara na badala yake watunze na kuhifadhi maeneo hayo kwa kuwa ni sehemu ya vivutio vinavyoingiza pato la Taifa kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo. "Pwani ya Mtwara imepata athari kutokana na watu wengi kutupa taka hususani mifuko ya plastiki na chupa za maji hali hii inatokana na watu wengi kutokuwa na elimu ya mazingira",alisema Okachu. Kauli hiyo imetokana na katibu wa Occupational safety Health and Environment (OSHE), Melessy Edward Okachu wakati akiongea na waandishi wa Habari katika ofisi yake iliyopo katika bandari ya Mtwara kuhusu ushiriki wao katika kuadhimisha siku ya Mazingira ambayo itafikia kilele chake tarehe 5 mwezi wa 6 mwaka huu. Aidha Okachu amesema kuwa tatizo la uchafuzi wa mazingira linatokana na wananchi kwa idadi kubwa ya wananchi wasio na elimu ya mazingira jambo ambalo amelitaja kuwa changamoto inayotakiwa kufanyiwa kazi kwa haraka. Tafiti zinaonekana kuwa asilimia kubwa ya upatikanaji wa maji yanatokana na uwepo wa mazingira yaliyojitosheleza kwa kukidhi mahitaji hivyo watu wanatakiwa kubuni njia mbalimbali za kukabiliana na uharibifu wa mazingira. Wakati wa uandaaji wa mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini (MKUKUTA wa kwanza na wapili) wadau wa mazingira walijalibu kubuni njia za kukabiliana na uhalibifu wa mazingira mbinu hizo zililenga kupunguza idadi ya watu wanaotuma kuni na mkaa asilimia 90 hadi 80. Aidha athari zinazotokana na kuwepo uharibifu wa mazingira n pamoja na uharibifu wa tabaka la hewa ya ozone, magonjwa ya ngozi , ongezeko la Joto , ukame na mabadiliko ya tabia ya nchi.
|
Men should take care of the environment And ASIA KILAMBWANDA, Mtwara Mtwara Region Citizens are required to uselessly kutotupa particularly in coastal sea port of Mtwara and instead develop closer and storage areas that are part of the attractions vinavyoingiza GDP for the current and future generations. "Coast of Mtwara has many side effects due to litter, especially plastic bags and bottles of water this is because most people have no knowledge of the environment", said Okachu. Statement is based on the Secretary of Occupational Safety Health and Environment (wash), Melessy Edward Okachu while speaking with journalists of the news in his office located in the port of Mtwara about their participation in the celebration on the Environment, which reaches its peak on the fifth month of the sixth year this. Moreover Okachu has said that the problem of pollution comes from people with large numbers of people without knowledge of the environment which mentions that the challenge needed to be worked on quickly. Studies seem to have a higher percentage of water supply due to the presence of conditions to meet the needs yaliyojitosheleza so people need to develop ways to cope with environmental degradation. During the preparation of the strategy of promoting economic growth and reduce poverty (MKUKUTA's first and second) stakeholder environmental jalibu develop ways of dealing with uhalibifu environment these techniques aimed to reduce the number of people who sent wood and coal 90 percent to 80. Also the effect caused by the presence of environmental damage and degradation of n with the air of the ozone layer, skin diseases, increased temperature, drought and climate change.
|
Translation History
|