Envaya

/m-e-d-1-1/news: English: WIXQJyE2lsQIt2AlywwLdXUE:content

Base (Swahili) English

 

WAKETI KWENYE UDONGO DARASANI KWA UHABA WA MADAWATI

Wanafunzi katika shule ya msingi Chalula iliyopo Mvumi Makulu Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma wanakabiliwa na uhaba wa madawati na kusababisha kuketi chini huku baadhi ya madarasa yakiwa hayana sakafu.

Hayo yalibainika hivi karibuni wakati wa ziara iliyofanywa na shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) ambapo lengo  lilikuwa kufuatilia mradi wa ‘Haki zangu Sauti yangu’ unaotekelezwa katika shule 20 zikiwemo shule 16 za  Msingi na 4 za Sekondari zilizopo  wilaya ya chamwino pamoja na ufuatilaji wa matumizi ya maendeleo ya vitabu walivyotoa msaada katika shule hizo.

Kwa mujibu wa Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Amina Mohamed, hali ya madawati katika shule hiyo ni mbaya kwani imefikia hatua wanafunzi wa darasa la tatu kuketi chini kwenye udongo kutokana na darasa kutokuwa na sakafu na kuwepo kwa msongamano wa wanafunzi 150 katika darasa moja.

Licha ya kuishukuru MED kwa kutoa msaada wa vitabu 1015 vya kiingereza, Hisabati na Atlasi katika shule hiyo, mwalimu huyo alisema kuwa mahitaji ya vitabu bado ni makubwa. Changamoto nyingine katika shule hiyo ni hali mbaya ya uchakavu wa majengo yasiyo na milango.

Tatizo la upungufu wa madawati imewakumba pia wanafunzi wa shule ya Msingi Mvumi Makulu kutokana idadi ya  madawati 100 waliyo nayo kati ya madawati 407 yanayohitajika.

Mwalimu mkuu wa Shule hiyo, Mary Mabichi alisema wanakabiliwa na upungufu wa madawati 307 na vyumba vya madarasa ni vidogo hali inayosababisha wanafunzi kuketi kwa kusongamana. Alisema kuwa walijitahidi kushirikisha jamii ili kuweza kupunguza ukubwa wa tatizo hilo na waliweza kuchangia madawati 40.

Mabichi alisema wanafunzi wengi wanakaa wakiwa wamesongamana na madawati hayo yako katika madarasa mawili kati ya saba yaliyopo ambapo dawati moja hukaliwa na wanaafunzi watatu hadi wanne.

Alisema kuwa darasa la sita na saba huketi kwenye madawati huku madarasa yaliyobaki wanafunzi wanakaa chini. Pia alisema wanafunzi wa chekechea wamepewa madawati 10 ili wasione taabu kuja shuleni kwani wakati mwingine kukaa chini kunasababisha baadhi ya wanafunzi kuchukia shule.shule hiyo ilipokea jumla ya vitabu 1036 kutoka shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma.(MED)

SOIL CLASS sat on benches shortages

Students in elementary school Chalula existing rumors Makulu Chamwino District in Dodoma are faced with a shortage of desks and cause to sit down with some classes being not contain floor.

That yalibainika recently during the visit made ​​by the organization Friends of Dodoma Education (MED) where the target   was to monitor the project's 'My Rights My Voice' is implemented in 20 schools, including 16 schools of   Elementary and Secondary 4 available   Chamwino district with the use of development ufuatilaji books were provided assistance in these schools.

According to the head teacher of the school, Amina Mohamed, the desks at school is bad because prevalent steps Grades of three sat down on the ground due to class no floor to the presence of congestion of students 150 in the same class.

Despite MED tribute to the 1015 books provide support for English, Mathematics and Atlas at the school, the teacher said that the needs are still great books. Another challenge in the schools is the poor state of deterioration of buildings without milan go.

The problem of shortage of desks are also a reality for primary school students Speculation M Akulu from a number of   100 desks desks that they have between 407 required.

The head teacher of the school, said Mary raw faced with shortage of desks DAR 307 rooms are tiny parties resulting in pupils sit crowded. He said that they tried to engage the community in order to reduce the size of the problem and were able to donate 40 desks.

Green said many students lived in crowded and these desks are in two of the seven classes available where one desk is dominated by three to four discipleship.

He said that the sixth and seventh grades sit on benches while the remaining classes students sat down. He also said the kindergarten students were given 10 desks so that they see trouble coming to school because sometimes sit down causes some students hate shule.shule it received a total of 1036 books from the Friends of Education organization Dodoma. (MED)


In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register

Translation History

Google Translate
April 14, 2013
SOIL CLASS sat on benches shortages – Students in elementary school Chalula existing rumors Makulu Chamwino District in Dodoma are faced with a shortage of desks and cause to sit down with some classes being not contain floor. – That yalibainika recently during the visit made...