Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

1. Katika kuzuia wimbi la vijana kujiingiza  katika matumizi ya madawa ya kulevya ,Tosa inatoa elimu kwa vijana jinsi ya kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya madawa ya ikishirikiana na wadau mbalimbali.

2 Tosa inawasaidia watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira hatarishi  kuendelea na masomo kwa kuwapa sare za shule na vifaa vya shule mara 2 kwa mwaka

3.Kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa wajane, vijana na walezi wa watoto ili waweze kutumia raslimali walizonazo kuboresha maisha yao.

4.Tosa inatoa  semina  kwa waalimu wa shule za msingi ili kugundua mabadiliko ya tabia za watoto wanaishi katika mazingira hatarishi  ili kuweza  kwasaidia na kuwapa ushauri.

5.Tosa inafanya  mradi wa mama na mtoto kwa kushirikiana na  shirika la tandabui healthaccess Tanzania ili kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto chini ya miaka 5  katika kutoa elimu kwa jamii katika wilaya ya nyamagana kupitia kwenye zahanati na mikutano ya jamii.

6.Tosa  inatoa elimu juu ya mabadiliko ya tabia katika vita dhidi ya malaria katika wilaya ya nyamagana kwa kushirikiana na shirika la  tandabui la mwanza na  mtandao wa kuthibiti malaria-  tanam  dar es salaam.

7. Tosa inatoa elimu ya makuzi kwa watoto ili kuwaanda  ili  kuweza kukabiliana na mabadiliko ya mwili  kupitia vikundi vya watoto  na michezo