Envaya

tosa inafanya kazi katika shule za msingi kwa kushirikiana na waalimu na viongozi wa mitaa ili kupata habari sahihi kuhusu watoto wanaohitaji kufadhiliwa na shirika letu

tosa pia inafanya uchunguzi ili kujua wahitaji walio na hali ngumu zaidi na kuwapa kipaumbele.pia inafatilia afya za watoto hao kwa karibu na  mahitaji ya chakula inapotokea uhitaji huu.

tosa inatajia kuwasiliana na RITA ili watoto yatima  na wanaoishi kwenye mazingira hatarishi wasajiliwe ili wapewe vyeti vya kuzaliwa.

kuendelea na kampeni za malaria kwa kufanya matamasha katika shule za msingi na kugawa vyandarua kwa wajane,watoto yatima na jamii zenye kipato kidogo

kuendelea kuwaelimisha jamii juu ya haki za wajane  na watototo yatima kwa kupitia

vipeperushi,mikutano,makongamano na vyombo vya habari.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

10 Machi, 2011
Ifuatayo »

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.