Injira
TANZANIA SCIENCE JOURNALIST ASSOCIATION

TANZANIA SCIENCE JOURNALIST ASSOCIATION

DAR ES SALAAM, Tanzania

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

TASJA yapata viongozi wapyaMgeni Rasmi akifungua Mkutano Mkuu wa uchaguzi wa Uchaguzi wa TASJA, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk. Hassan Mshinda, akitoa hotuba ya ufunguzi, kushoto ni Meneja Mkuu wa Biashara na uwakala wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kilala Sendama.Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa TASJAMjumbe wa Mkutano Mkuu wa TASJA, na Katibu Mtendaji Mstaafu, David Ramadhan akichangia hoja katika mkutano wa uchaguzi.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

CHAMA cha Waandishi wa habari za Sayansi nchini (TASJA), kimepata viongozi wapya watakiongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo

Waliochaguliwa ni Pamoja na Greyson Mutembei, ambaye ni Mwenyekiti mpya, Bakari Kimwanga Makamu Mwenyekiti, Benard Lugongo Katibu Mkuu na Nasra Abdallah Mweka hazina.

Mbali mkutano huo umewachagua wajumbe wa kamati ya utendaji ambao ni David Ramadhan, Asia Rweymamu, Gabriel Mushi, Restusta James, Jackob Nduye na Hamis Shimye.

Awali akifungua mkutano Mkuu huo wa mwaka, mgeni rasmi ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk. Hassan Mshinda, alisema ili nchi iweze kuendelea inahitaji wanasayansi na wabunifu wengi ambao wataleta maendeleo nchini.

“Tunajua TASJA kwa namna mlivyo mnaweza mkawa chachu ya maendeleo katika sekta ya Sayansi nchini, nasi kama wadau wakuu tunaamini waandishi wa habari mna mchango mkubwa katika wakuelimisha wananchi.

“Ahadi yangu kwenu TASJA kupitia COSTECH mnafika mbali sambamba na kuwaunganisha na taasisi zingine kimataifa,” alisema Dk. Mshinda

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Biashara na uwakala wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kilala Sendama, alisema kuwa hivi Maendeleo ya teknolojia za mawasiliano yamejkuwa yakichukua nafasi kubwa katika maendeleo ya Taifa.

“Kwetu TPC tumejiandaa katika kutoa huduma zatu ikiwemo EMS, Post Cargo na Inateranet ambayo imekuwa ikitumiwa na watanzania wetu nanyi TASJA ni moja ya wadau wetu,”alisema

17 Mutarama, 2013
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.