Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

2. MKUTANO MKUU WA MWAKA WA MARAFIKI WA ELIMU TANZANIA

Siku ya tarehe 01 Septemba 2010 hadi 03 Septemba 2010, kwenye ukumbi wa VETA Dodoma, kulifanyika mkutano mkuu wa Marafiki wa Elimu Tanzania. Mkutano huo uliitishwa na shirika la hiari la HakiElimu. Kwa mujibu wa taarifa ya waandaaji wa mkutano huo, walielezea kuwa mkutano huo ulihudhuriwa na Wanaharakati wa Marafiki wa Elimu wengi zaidi kuliko mikutano mingine iliyotangulia.

Jumla ya washiriki zaidi ya mia moja walihudhuria mkutano huo. Miongoni mwa wanaharakati waliohudhuria mkutano huo, alikuwemo Mratibu na Mshauri wa kikundi cha Wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya - WEMA, Mr. Mussa P.M. Kamtande.

Kwenye picha anaonekana Mratibu na Mshauri wa kikundi cha WEMA, Mr. Mussa P.M. Kamtande akisisitiza jambo, wakati alipopata nafasi ya kuelezea na kutoa uzoefu wake wa namna kikundi chake cha WEMA kilivyoweza kufanikiwa katika shughuli zake.

Mambo ambayo yameweza kufanywa na kikundi cha WEMA katika kipindi cha miaka mitatu toka kuanzishwa kwake mwezi Januari 2008, ni pamoja na ; Kuanzisha Maktaba ya Jamii Mkalapa, baadhi ya vitabu na machapisho yalitolewa na HakiElimu. Ujenzi wa ubao wa matangazo karibu na ofisi ya kijiji cha Mkalapa, mradi pia uliofadhiliwa na HakiElimu. Kuendesha mijadala ya wazi ambayo nayo ilifadhiliwa na HakiElimu, na Kuendesha vipindi vya redio kupitia redio Pride fm 87.8 ya mjini Mtwara, ambapo marafiki wa elimu kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi walishirikishwa. Kati ya mwaka 2009 na mwaka 2010 jumla ya vipindi 23 vilirushwa hewani kupitia kipindi chake maarufu cha "Joto la Wiki" kinachorushwa na redio Pride fm 87.8, kila siku ya Jumapili kuanzia saa 10.15 hadi saa 12.00 jioni.

Kikundi cha WEMA kimefanikiwa pia kuunda vitengo ambavyo lengo lake ni kuwawezesha watu mbalimbali kushiriki katika mafunzo ya ujasiliamali. Kitengo kimojawapo kinajulikana kama; WEMA ART AND CARPENTRY SKILLS PROMOTION ama kwa kifupi; "WACS-Promotion." Kitengo hiki kinajishughulisha na kutoa mafunzo ya aina mbalimbali yakiwemo mafunzo ya useremala, uchoraji na uchangaji vinyago, pamoja na ujasiliamali. Kitengo hiki licha ya kwamba kinasimamiwa na WEMA, kitafanya shughuli zake chini ya Mchungaji Joseph Mwanga, mtaalamu wa seremala kutoka chuo cha ufundi VETA Ndanda.

Kitengo kingine kilichoundwa na WEMA kinajulikana kama; WEMA WOMEN EMPOWERMENT GENERATION, ama kwa kifupi,"WEMA Women-EG". Kitengo hiki kimelenga kuwahamasisha akina mama ambao ndio mhimili mkuu wa familia,ili waweze kushiriki katika harakati mbalimbali za kiuchumi. Katika hatua za awali,WEMA Women-EG wameanza kujifunza utengenezaji wa vyungu vya kupandia maua.

WEMA Women-EG wameanzisha timu za mpira wa pete na wavu kwa ajili ya wasichana, chini ya ufadhili wa; "Sports Development Aid (SDA)" kupitia mradi wake wa; "Mother & Daughter Project". Mradi wa 'Mother & Daughter Project' umelenga kuhamasisha akina mama wapate nafasi ya kufanya mazoezi madogo madogo kwa ajili ya kujenga afya zao. Tafiti nyingi zilizofanyika, zimedhihirisha wazi kwamba akina mama wengi katika nchi zinazoendelea kama Tanzania, wakati wote huwa kazini, na kwamba hawapati muda wa kupumzika. Katika hatua za awali, shirika la hiari la SDA chini ya mradi wa "Mother & Daughter Project" wametoa mipira kwa timu hizo mbili kwa ajili ya mazoezi.

Pamoja na mambo hayo yote, kitengo kinakusudia kuwapatia akina mama mafunzo ya; utaalamu wa utengenezaji wa batiki, utaalamu wa ubanguaji wa korosho pamoja na ufugaji wa kuku wa kienyeji. Aidha, WEMA Women-EG wanakusudia kutembelea taasisi zilizopo katika Kata ya Mwena wilaya ya Masasi ili kuongea na wanafunzi wa kike juu ya umuhimu wa mtoto wa kike kuwa na elimu, pia kuwakumbusha athari za miba za utotoni kwa msichana. Aidha, lengo la baadaye wakiwa na uwezo ni kutembelea taasisi nyingi zaidi katika wilaya ya Masasi.

Kikundi cha WEMA kimesajiliwa rasmi chini ya CBO's na mpango wa baadaye ni kukisajili kuwa NGO. Kikundi kina Katiba pamoja na Mwongozo unaotoa mwelekeo wa mambo yanayoshughulikiwa na yale yanayotarajiwa kushughulikiwa. Wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya - WEMA wanayashukuru mashirika yote ya hiari ambayo yamekiwezesha kikundi kupiga hatua katika kutekeleza malengo iliyojiwekea

October 13, 2010
« Previous Next »

Comments (1)

NASHON DAVID (DODOMA) said:
I am actually very happy noticing your progress in the lovely campaingn of right for education, especially to our young and slowly growing economy. I too understand the values of keeping pronouncing the integrity and stabilization of education in our country. Thank you guys for a nice handsome work
November 18, 2011

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.