Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations
Lowassa Akuatana na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto kujadili sababu za kufanya vibaya kwenye mtihani wa Taifa


Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza kwa kusisitiza wakati wa mkutano wake na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto,Wilayani Monduli kuhusiana na hali ya elimu katika shule hiyo kutoridhisha na kupelekea wanafunzi wengi wa shule hiyo kufeli kwenye mtihani wa taifa wa kidato cha nne.Mkutano huo umefanyika leo shuleni hapo,ambapo walimu wa shule hiyo walitoa changamoto mbali mbali wanazomabiliana nazo.Mh. Lowassa amewaasa walimu wa Shule hiyo kuwa wafanye kazi kwa juhudi ili kuwaandaa vijana wa taifa la baadae.Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo,Bw. Joseph Lukumay.










Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimsikiliza kwa makini,Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Shule ya Sekondari ya Engutoto,Bw. Joseph Lukumay.
Picha na habari na Blog ya HakiNgowi