Envaya

HakiElimu

Amakuru

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations
Haki Elimu HakiElimu

Tuungane watanzania kujadili bajeti ya wananchi na wadau wa elimu wakati bajeti ya elimu ikisomwa bungeni mkutano unaanza #bajetielimu

Haki Elimu HakiElimu

Kisha kutakuwa na uchambuzi wa bajeti ya elimu itakayosomwa bungeni leo wadau wote mnaombwa kufuatilia na kushirikiana #bajetielimu

Haki Elimu HakiElimu

Habari za asubuhi watanzania, wakati bajeti ikitarajiwa kusomwa leo bungeni tuna mkutano na wadau wa elimu kujadili matarajio #bajetielimu

Haki Elimu HakiElimu

dozens of people followed me and 5 people unfollowed me // automatically checked by http://t.co/SaFvd1t8

Haki Elimu HakiElimu

Je bajeti ya elimu itakayosomwa bungeni jumatatu ijayo itatua changamoto hizi ?TAFAKARI... http://t.co/qwBWs1aI

Je Bajeti ya Elimu 2012/2013 itaboresha mazingira ya shule kama hizi.








IMG-20120724-00963.jpg
Shule hii ipo wilayani Muleba mkoani Kagera.
IMG-20120724-00967.jpg
Ndani ya shule hii licha kuwa ni shule yenye kuta na kuezekwa kwa nyasi, bali pia wanafunzi wanakaa chini
IMG_0261.JPG
Shule ya msingi Silabu wilayani Korogwe.Wanafunzi hawa wanasoma kwenye kichochoro kilichopo katikati ya madarasa mawili

Wanafunzi+wa+darasa+la+tatu+katika+Shule
 Shule ya msingi Silabu wilayani Korogwe.

MOJAWAPO+YA+MDARASA+YA+SHULE+YA+MSINGI+S
Shule ya msingi Selous iliyopo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma.

MWANDISHI+WA+HABARI+TOKA+STAR+TV+NA+RADI

WANAFUNZI+WA+MADARASA+MAWILI+SHULE+YA+MS

 Bajeti ya elimu itasomwa bungeni siku ya Jumatatu, 13 Agosti. Wakati bajeti ya Elimu inasubiriwa kwa hamu na wadau na hasa wapenda maendeleo ya Elimu, Baadhi ya maeneo nchini bado yanakabiliwa na changamoto kubwa sana hasa hali mbaya ya miundombinu, ukosefu wa vyumba vya madarasa na majengo ya shule ambayo yamesababisha baadhi ya shule kuweka madarasa ya nyasi kama shule ya msingi Selous na Mkapa zilizopo wilayani Namtumbo, Shule ya msingi Silabu iliyoko wilayani Korogwe, Shule ya msingi Misunkumilo ya wilayani Nkasi, na baadhi ya shule wilayani Muleba.

Hali ya elimu imezidi kuwa mbaya kila kukicha, kiasi kwamba hata watu hudiriki kuuliza kama shule hizo zipo nchini, hasa wakiangalia juhudi na kelele nyingi zilizopigwa juu ya mchango mkubwa wa MMEM na MMES kuwa zimefanya kazi kubwa sana kuboresha mazingira ya kujifunzia hasa miundombinu ya shule.Swali Je, shule hizi ziliachwa wapi na mipango hii? Je bajeti ya elimu ya 2012/2013 itatatua baadhi ya changamoto za elimu nchini?na kuondokana na majengo haya yasiyo rafiki kwa mwanafunzi na mwalimu?

 Mwana blog ya HakiElimu, Hebu angalia jinsi ambavyo wanafunzi huko Tanga,Rukwa,Kagera na Ruvuma wanavyojifunza kwenyesehemu zinazokatisha tamaa : Watatoka?


mojawapo+ya+darasa+shule+ya+msingi+selou
Shule ya msingi Selous iliyopo Namtumbo. Wanafunzi wa darasa la tano wakiwa darasani na mwalimu akifundisha.
  
Pix+35m+wanafunzi+wa+darasa+la+kwanza+ka
Wanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya Isensa ya wilayani Nkasi wakiwa darasa, darasa hili lina wanafunzi 211, mwalimu hana pa kukaa akifundisha hutoka nje kusubiri watoto wamalize kuandika.

Pix+85+na+88+wanafunzi+wa+shule+msingi+M
Wanafunzi wa shule ya msingi Misunkumilo ya wilayani Nkasi wakisoma kwenye darasa lililoezakwa kwa turubai, shule hiyo ina madarsa mawili ya namna hiyo ambayo yanatumiwa na wanafunzi wa darasa la tatu, la nne na awali.
IMG-20120723-00931.jpg
Shule hii ipo wilayani Muleba.
IMG-20120723-00953.jpg
Hiki ni choo cha shule wilayani Muleba

Haki Elimu HakiElimu

Wakati Waziri Mkuu akisema kuwa uamuzi wa kutotumia walimu hautokani na walimu hao kushiriki katika mgomo. Gazeti... http://t.co/SUK1T8Rc

Uhaba wa Madarasa: Wanafunzi wa Darasa la Tatu Korogwe Wasomea Uchochoroni




IMG_0261.JPG
Wanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi Silabu wakiwa darasani.
Darasa hili ni uchochoro uliopo shuleni hapo unaotenganisha jengo hadi jengo.

Wanafunzi+wa+darasa+la+tatu+wa+Shule+ya+
Wanafunzi wa darasa la tatu wa Shule ya Msingi Silabu wakitoa salamu 
kwa mwanahabari wa Thehabari.com alipowatembelea.

IMG_0264.JPG
Picha juu na Chini ni Wanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Silabu
 wakiwa kwenye darasa lao.
Baadhi+ya++walimu+wa+Shule+ya+Msingi+Sil
Baadhi ya  walimu wa Shule ya Msingi Silabu, wakiwa kazini

Mwalimu+Mkuu+wa+Shule+ya+Msingi+Silabu,+
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Silabu, Mizeki Charahani akiwa ofisini kwake.

 Na Joachim Mushi, Korogwe
WANAFUNZI wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Silabu iliyopo Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga wanasomea kwenye uchochoro unaotenganisha kati ya darasa moja na lingine kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa.
Wanafunzi hao ambao darasa lao limekuwa likihama kila muda kutengemea hali ya hewa (jua na mvua) kufuata kivuli wamelazimika kusomea nje kwenye uchochoro ambao haujaezekwa kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa shuleni hapo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni katika shule hiyo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Silabu, Mizeki Charahani alisema wanafunzi hao wamelazimika kusomea nje kwa kuwa wanavyumba vinne tu vya madarasa ambavyo havitoshelezi kwa mahitaji ya shule.
Akifafanua zaidi alisema darasa hilo eneo lao maalumu la kusomea (darasa) ni kwenye uchochoro unaotenganisha kati ya darasa moja na lingine, lakini huwa wanahama jua linapozidi au mvua kunyesha na kwenda eneo lingine linalokuwa na kivuli.
“Darasa hili kwa kweli huwa linahama kulingana na hali ya hewa, jua likizidi wanabeba madawati yao na kuhamia eneo lenye kivuli, mvua ikinyesa hivyo hivyo wanahamia sehemu nyingine…lakini muda mwingine tunawahamishia kwenye darasa moja na wenzao pale kunapokuwa hakuna mwingiliano wa vipindi,” alisema Charahani.
Alisema shule hiyo yenye darasa la kwanza hadi la saba unauhaba mkubwa wa vyumba vya madarasa kwani hata darasa la kwanza na la pili wanasomea kwenye darasa moja kwa kupokezana.
“Kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa hata hatuna darasa la awali wala ofisi ya walimu…na sisi ofisi yetu ipo hapa chini ya mti huu,” alisema Mwalimu huyo huku akionesha eneo moja chini ya mti ulio mbele ya madarasa ya shule hiyo.
Akizungumzia hali hiyo, Ofisa Elimu Taaluma, Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Elius Mkwizu alikiri kuwepo kwa tatizo hilo la uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo na kudai shule hiyo ni mpya hivyo ujenzi wake haukwenda sambamba na ongezeko la wanafunzi kimadarasa.
Alisema tayari uongozi wa idara hiyo kwa kushirikiana na wananchi unafanya ujenzi wa madarasa mawili ambayo yatasaidia kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo. Hata hivyo aliongeza ujenzi huo kwa sasa umesimama baada ya fedha zilizotengwa kurejeshwa hazina kuu baada ya kukaa kipindi kirefu bila kutumiwa.
Mwandishi wa habari hizi alishuhudia moja ya ujenzi wa darasa lililosimama baada ya kukosekana kwa fedha za kuliendeleaza. Akifafanua zaidi Mkwizu alisema kulikuwa na mvutano kati ya viongozi waliokuwawakisimamia ujenzi huo na wananchi hali iliozua mgogoro na ujenzi kusimama.

Habari hii imeandaliwa na gazeti tando la www.thehabari.com kwa ushirikiano na HakiElimu

Haki Elimu HakiElimu

Bajeti ya elimu itasomwa bungeni siku ya Jumatatu, 13 Agosti. Ungependa ibebe mambo gani muhimu? Hali ya elimu... http://t.co/VnpyiPFS