Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) ni chama kilichoanzishwa na Viziwi wenyewe mwaka 1983 na kusajiliwa rasmi na Wizara ya Mambo ya Ndani tarehe 04/09/1984 na kupewa no so. 6466 na baaada ya kupitishwa kwa sheria ya Uanzishwaji wa vyama vya kiraia ya mwaka 2002, CHAVITA ilipata hati namba NGO 1878 tarehe 21/04/2006.
Kwa sasa CHAVITA ina Matawi 18 kwenye Mikoa 18 ya Tanzania bara ambayo ni Mwanza Shinyanga, Mara, Kagera, Dodoma, Tabora, Kigoma, Arusha, Tanga, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Morogoro, Pwani, Mtwara, Kilimanjaro,Lindi na Dar Es Salaam.
CHAVITA Tawi laWilaya ya Dodoma mjini lilianzishwa May 2011, toka kuanzishwa kwake limekuwa likiunua maisha ya Viziwi wa Wilaya ya Dodoma katika kupiga vita Umaskini na Unyanyampaa pamoja na kupigani a haki zote za kibinadamu kwenye nyanya zote za maisha ya Viziwi zikiwapo shughuli za mapambano dhidi ya kuenea kwa Maambukizi ya VVU/UKIMWI na kutoa ushauri nasaha kwa waathirika Ili kufanikisha shughuli za utetetezi na ushawishi na kuhakikisha kwamba Viziwi wana Maisha bora