Maisha ya Kijiji,wakati mwingine kutokana na ukosefu wa vifaa mbalimbali vya kurahisisha shughuli zako za kila siku za kujiongezea kipato kama vile trekta,plau dhana inayotumika katika kilimo au jembe la kukotwa kwa Ng'ombe au wanyama pia hata hukosa mwevuli wa kujikinga na mvua pindi mvua inyeshapo,hutumia jani la Mgomba kujikinga na mvua,hapa Mkurugenzi Mtendaji wa CHACODE,Thadei Hafigwa ili kuendana na mazingira ya Kijiji amelazimika kutumia Jani la Mgombea kujikinga na mvua.
Kiwango cha maisha ya watanzania walio wengi ambao huishi vijijini wanajenga nyumba zao kwa kutumia dhana za asili,nyasi zinatumika kujenga na kuezeka.Tanzania ina safari ndefu ya kuhakikisha ya kuwa kila mtazania anaishi katika nyumba bora na ya kisasa,mlo wake si wa kubahatisha,watoto wanakwenda shule,wanafunzi wanafundishwa vema na walimu wao walioandaliwa mazingira mazuri ya kufundisha.
baadhi ya maeneo vijijini wanajikuta bado wanatumia kinu na mche kutwanga nafaka ili waweze kupata unga utakaotumika kuandaa chakula chao,hii inatokana kukosekana na kwa wawekezaji wa kupeleka mashine za kusaka nafaka.