Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations
VIGODORO/ RUSHAROHO Nimarufuku kwenye sherehe za kiislam GAIRO. Hayo yalisemwa na sheikh wa kata ya Gairo Sheikh Nassoro Bakari baada ya kumalizika kikao cha baraza la masheikh kata ya Gairo. Akitoa taarifa hiyo makamu wa Imam wa msikiti wa Wilaya ust. Yusuf alisema, Hairuhusiwi kwa Mislam kuhusisha sherehe za kidini na miziki. Hata hivyo amesama atakaekiuka masheikh hawata fika kwenye shughuli yake na atatengwa katika maswala ya kidini ikiwa ni pamoja na kutofika kwenye msiba unaoihusu familia yake. Msumeno huo utamkumba pia Sheikh atakae shiriki kwenye mkumbo huo, ni msimamo mkali ambao sheikh wa Wilaya pia ameunga mkono na kupendwa na waislam wanaozingatia dini.
May 17, 2014
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.