Tumeamua kujikita katika shughuli za kilimo hususani kilimo cha bustani na ufugaji wa kuku. Ni dhamira yetu kuhakikisha kuwa jamii inapata lishe bora na salama kwa afya, ni fahari kwetu kuona kuwa vijana wanaelimika na kuchagua mfumo wa maisha kiuchimi kupitia rasilimali zinazo wazunguka kama nyezo ya kuwainua kiuchumi, jamii inahitaji nyama ya kuku na mazao mengine ya kuku kama Mayai na mbolea ya kinyesi cha kuku. Mazao haya ya kuku ni frusa kwa vijana kwani wakielimishwa na wakawa tiari kuwekeza katika sekta ya ufugaji kupitia Ndege jamii ya kuku watakuwa wamekubali kutatua Matatizo yaliyopo katika jamii yatokanayo na uhaba wa mazao ya kuku. Sisi kama ASASI ya AUVITA tumejidhatiti kwa dhati kuwekeza kwa vijana wa Tanzania ili kuwawezesha kukabiliana na uhaba wa ukosefu wa ajira. Takwimu zonaonesha kuwa idadi ya watu inazidi kuongezeka kila leo na watu Hawa wanahitaji kula na wenyejukumu la kuwalisha ni sisi vijana kwa kuwekeza katika sekta ya kilimo. Hivyo tukiwa kama vijana tunatoa rai kwa watanzania vijana kuwekeza katika sekta ya kilimo ili kujikwamua kiuchumi na kukidhi nahitaji ya Chakula. Pichani ni kuku wa Kienyeji walioboreshwa kwenye asili ya India.
May 21, 2017