UFUNGUZI TAWI JIPYA
Napenda kuwapa taarifa wadau na wanaharakati wote kuwa Makao makuu ya Voyohede Mtwara yamekubari ombi la kufungua tawi jipya Dar es salaam kwa mkataba maalumu ambao utasainiwa na wanachama wa Dar ambao ofisi na eneo la mradi lipo kule Tabata kisukuru. Hivyo wabia wa asasi hii mnachaguo la wapi muende. Muongozo au mpango mkakati wa VOYOHEDE makao makuu unatambua uwepo wa tawi moja ambalo litafuata taratibu zilizopo katika mkataba, lengo lakuwa na matawi machache ni kwa kuwa uwezo wa kuwawezesha na kuwaongoza wanachama wa tawi husika ni mdogo na kwa hiyo basi shughuli hii itafanyika kwa kuzingatia uwezo na maslahi ya pande zote mbili yani makao makuu na tawini. Matawi yatajitegemea kwa kila jambo maelezo na miongozo yao kabla ya kutekelezwa yatatakiwa yakubaliwe na wanachama wa tawi husika bila kuvunja mkataba wake na makao makuu. VOYOHEDE-MAKAO MAKUU MTWARA inaona ufunguzi wa tawi hili la Dar es salaam ni fursa kubwa kwao na kwa tawi hivyo inaomba ushirikiano na upendo kama ndugu wa familia moja.
Nawatakia mafanikio mema,
Wenu,
Afisa Habari na Utawala
VOYOHEDE-TANZANIA
Mratibu wa mradi wa UMESE akipata maelezo na maLekebisho ya mradi kutoka kwa wawezeshaji
Mhasibu na Mratibu wa mradi wa UMESE wakifuatilia kwa makini mafunzo ya usimamizi wa mradi kule Dodoma
UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAFUNZO YA JKT KWA WANAOMALIZA KIDATO CHA SITA NI KUWEKA MATABAKA.
Itakumbukwa kuwa ongezeko la idadi ya watu Tanzania ni kubwa sana,na miongoni mwao ni vijana, wakati serikali inakabiliwa na changamoto ya kuwawezesha vijana kiuchumi kwa kuwahakikishia elimu ilio bora limekuja wazo la kuwapeleka vijana JKT kwa mujibu wa sheria, vijana hawa ni wale tu waliofaulu kidato cha sita wakapata daraja la kwanza na la pili na wale waliopata daraja la tatu kwa michipuo ya sayansi. Kundi hili ni dogo sana ukilinganisha na idadi ya vijana waliomaliza kidato cha sita kwa mwaka 2013 tu.
Mafunzo ya JKT ni muhimu kwa watanzania wote kutokana na faida zinazotokana na mafunzo haya, kwa ufupi tu mafunzo ya JKT humfanya kijana aweze kufanya kazi au kuishi katika mazingira yoyote ambayo binadamu anaishi, yanamfanya kijana kuwa na utii na kujali watu kikamilifu pia yanafanya kijana kuweza kujitegemea na kukabiliana na shida mabalimbali zinazomkabili na zaidi mafunzo haya huongeza uzalendo kwa raia. Hizi ni baadhi tu ya faida zinazopatikana kwa mtu binafsi. Lakini zipo faida ambazo taifa linaweza kuwa nazo kama vijana wake wanapatiwa mafunzo haya, mfano kuwa na taifa lenye watu waliokuwa tayari kwa ulinzi wa taifa lao, kuzalisha mali kwa gharama nafuu kwa kutumia askari vijana waliopo makambini na kuboreka kwa huduma zinazotolewa na waajiriwa ambao wamepitiamafunzo haya ambao hujali muda na wateja wao wanaowahudumia.
Faida hizi na nyingine nyingi serikali iliziona na ndio maana ikaweka mpango huu ambao hatujui kama utakuwa endelevu na kama utakuwa endelevu, je? Utakuwa endelevu kwa makundi yapi yaani yenye sifa zipi? Kwa utekelezaji unavyoendelea hivi sasa mpango huu mzuri na wa kizarendo kwa taifa letu utaleta matabaka makubwa mawili ambayo ni hatari kwa usalama wa taifa hapo baadae. Serikali inabidi ikumbuke kuwa mpango huu umeanza 2013 na ni kwa wanafunzi baadhi tu ya waliofaulu kidato cha sita, hivyo ni kundi dogo sana kwa kuwa tunajua wapowaliofeli na wapo walio faulu na waliofeli ambao ni wa miaka ya nyuma na hili ndilo kundi kubwa sana.
Tunaishukuru sana serikali kuurudisha mpango huu muhimu na mzuri kwa taifa letu hasa ukilinganisha na changamoto zinazolikabili taifa hivi sasa, changamoto za uuzaji, usafirishaji na utumiaji wa madawa ya kulevya, ushabiki wa kisiasa, rasilimali, uwajibikaji mdogo na ongezeko la watu. Mpango huu unaweza kugusa kila aina ya changamoto hizi na kuzipunguza kwa kiwango kizuri sana lakini tu kama kutakuwa na uwiano wa kuwapeleka mafunzo haya ya kijeshi vijana wote wenye fursa na wasio na fursa, nikiwa na maana wale weye sifa za kujiunga na vyuo na wale wengine wowote waliopo majumbani na mitaani bila shughuli yoyote. Kwa kufanya hivi hatutaweza kulijenga taifa lenye matabaka ya walio na uwezo na wasio na uwezo. Tunajua upungufu wa rasilimali zinazoweza kuwezesha makundi haya yote kwenda jeshini, lakini serikali inaweza kuanza kwa awamu nusu wakachukuliwa wale tu waliopata fursa ya kumaliza kidato cha sita na nusu wengine wale ambao hawakupata fursa ya kufika kidato cha sita yaani darasa la saba na wote waliofeli kidato cha nne. Hivi tunaweza tukaenda mpaka tukafika wakati uwezo wa kuwapeleka makundi yote haya mawili walioko mitaani na wanaomaliza kidato cha sita ikawezekana.
Kwa kuendelea kuchukua wanaofaulu kidato cha sita peke yake na kuwaacha wengi waliofeli darasa la saba na kidato cha nne na waliofeli kidato cha sita jumuisha na waliokuwapo tiyari mitaani toka miaka ya nyuma, huku ni kuweka MATABAKA ambayo dhahili yatakuwa yanatofautiana KIUCHUMI na KIELIMU. Vijana ambao wameishia darasa la saba na wamefeli kidato cha nne wakipatiwa mafunzo ya JKT ni fursa kubwa sana kwao, maana wanaweza kujiunga na makampuni ya ulinzi, wanaweza kujishughulisha na kilimo au ujasilia mali, wengine wanaweza kujiendeleza kielimu na fursa nyingine nyingi ambazo wanaweza kuzipata kutokna na cheti au mafunzo ya JKT, hali kadhalika kwa wanao maliza kidato cha sita na kukosa nafasi za kuendelea na elimu ya vyuo. Lakini kundi hili likiachwa ni kujitengenezea migogoro na migomo na hali ngumu ya maisha kwa vijana hawa, tunaona na tutaendelea kuona ongezeko la vijana wanaotumia madawa ya kulevya, miashara ya ngono, wizi,ujambazi na hata ugaidi. Taifa litakuwa halina amani na halite tulia, serikali itatumia gharama kubwa katika kuimalisha ulinzi na kutawala watu wake lenyewe. Wakati kundi hili la wasomi na lililopata fursa ya kupitia JKT litakuwa na uwezo kiuchumi na elimu, na makundi haya mawili hayataweza kukaa katika mtaa mmoja kwa kuwa yatakuwa makundi hasimu nao pia watatumia gharama kubwa kuishi kwaajili ya kuijiimalishia ulinzi na usalama wa wao na familia zao. Inawezekana serikali ilianzisha mpango huu ikiwa inataka kumaliza kwa haraka tatizo la migomo ya vyuo vikuu iliyoibuka miaka ya hivi karibuni ama kuboresha utoaji wa huduma katika taasisi za serikali, lakini hilo sio suluhisho pekee, suluhisho la jumla ni kuhakikisha makundi yote ya vijana waliopata fursa ya kusoma na amabo hawa kupata fursa hiyo wana kwenda kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa uwiano ulio sawa na kwa hivyo ili nchi iwe na amani ya kweli ni razima kuwe na usawa katika mgawanyo wa rasilimali na fursa, kulingana na nafasi waliokuwa nayo raia sehemu husika.
Maoni yangu katika mpango huu wa serikali kupitia Jeshi la kujenga taifa ni kuhakikisha kwanza vijana wote wasio kuwa na kazi na hawakusoma na wapo wanazurula mitaani wanapelekwa jeshini kwa mujibu wa sheria ili kupunguza matatizo mengi ya kijamii, kisiasa na kiuchumi yanayoweza kutokea katika jamii, ndipo wafuate wasomi ambao nao tunakubali ni lazima wakahudhuria mafunzo haya ilikuboresha utoaji wa huduma za jamii. Serikali itakapo kuwa na rasilimali za kutosha makundi haya yawe yana kwenda katika mafunzo ya JKT kwa uwiano ulio sawa au mpango huu kwa sasa utekelezwe moja kwa moja kwa uwiano sawa kwa makundi haya makubwa mawili yote kwenda jeshini kwa pamoja, kuliko inavyo fanyika hivi sasa huku ni kuweka matabaka katika jamii ya watanzania ambao ni wamoja na wanatenganishwa katika huo umoja kwa mifumo kama hii isiyochambuliwa kwa kina kabla ya utekelezaji wake.
Wenu,
Deogratius Makoti
MWANAHARAKATI WA MASWALA YA VIJANA NA AFYA.
Mob: 0714113952/0782956772
Siku ya vijana duniani, serikali imeainisha mikakati na sera za kuwakwamua vijana?
Nilikuwa kimya nikisikiliza na kufuatilia kwa makini matamko au hutuba zenye mantiki kwa vijana wa Tanzania kutoka serikalini. Nilianza kwa kuingia mtandaoni labda kunachochote nikakaa karibu na redio na kila wakati wa habari nilibadilisha kituo mara hiki mara kile ilimladi nisikie hotuba ya kiongozi yeyote wa serikali akitamka jambo kwa vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa lolote duniani. Mpakailipo malizika taarifa ya habari ya saa mbili usiku ya moja ya redio kubwa hapa nchini ndipo nilipo pandisha na kushusha pumzi na kuanza kufikiri kwa kina zaidi.
Hivi serikali, taasisi na idara zake haitambui siku ya vijana duniani? Na kama inatambua inaienzi vipi siku hii? Au inaitumiaje? Au ndio haifanyi maadhimisho mpaka waisani mashirika yasio ya kiserikali yanayojihusisha na mambo hayo yaoneshe nia na kuadhimisha siku hiyo kwa ushirikiano na serikali kama tunavyoambiwaga? Hapa naizungumzia serikali ngazi ya Wizara na Idara makao makuu, lakini kule mikoani katika ofisi za Katibu tawala wa mikoa kuna wataalam walioajiriwa miaka ya hivi karibuni kama watu wanaoshughurikia maswala ya michezo na maendeleo ya vijana. Hawa tutasema wapo chini ya serikali kuu hawana bajeti ya maendeleo, na vipi katika ofisi za Wakurugenzi wa halmashauri zetu?
Kama wanamipango wanatumia wakati gani kutoa taarifa kwa watu wa kawaida? Kama ipo na ni hafifu, wataalam watasema vipau mbele, ama mipango tuliopanga kwa mwaka wa fedha haikupitishwa, niwakati gani sisi vijana tutajua haya? Amana katika mbao za matangazo pale halimashauri ni matangazo ya kawaida tu, tunashukuru kwayo maana tukitaka taarifa hizo tunazipata hapo. Ama taarifa hizi za utekelezaji wa maendeleo kwa vijana na mipango yake au sera zinazomuwezesha kijana hasa kijana wa kawaida tunazipata wapi?
Hivi sasa Tanzania kunajuhudi kubwa za utumiaji(Utilization) ya mali asili kama Gesi, Madini, Bahari, Maziwa na Mito. Katika Gesi peke yake nina imani kuwa vijana wengi waliosoma na wasio soma wanaweza kupata fursa, Madini halikadhalika na Maji kwa maana ya mito, maziwa na Bahari kwa mfano halimashauri zilizo chini ya mamlaka ya kuliendeleza bonde la mto kilombelo zimejipanga vipi kujenga fursa kwa vijana waishio katika mradi ulio chini ya mamlaka hizi? Wanatumia muda gani kuwafahamisha vijana fursa zilizopo au zinazokuja kupitia mipango hii mikubwa ya maendeleo ya serikali? Mimi nilifikili fursa hizi zilizopo na zinazokuja serikali ingeweka kipaumbele hasa nafasi za ajira na fursa zinazotokana na mipango kama hii kwa vijana, na siku za maadhimisho ya siku ya vijana duniani, Halmashauri kama Halmashauri au Mkoa kama Mkoa hata serikali kuu kwa ujumla inatumia nafasi ya siku kama hii kuelezea Mipango ya maendeleo kwa vijana iliyokwisha kutekelezwa au iliyopangwa kutekelezwa, hata kama kuna fursa vijana inabidi wapewe taarifa hii kwa lugha rahisi kwa kuwa ni haki yao ya kikatiba kupata taarifa.
Mamlaka zote zimekaa kimya najua kutakuwa na majibu mengi ya kisiasa, hatukuwa na bajeti, vipau mbele vilivyopitishwa ni vya shughuli za maendeleo tu na sio maadhimisho ya siku yoyote ile. Lakini hawa watu maalum(Focal Person) ambao ni wataalam mliowaajiri kazi yao ni nini? Je vijana wanataarifa ya sababu hizo? Je wameshirikishwa na imeshindikana? Na ninyi watumishi wa serikali mnaonaopewa dhamana hii mnafikiri vipi? Kuna fursa nyingi sana hata haziitaji kasma ya serikali kufanya shughuli ndogo kama hizi.
Ndipo nikaona kuwa UWAZI na UWAJIBIKAJI unatafsiri pana sana na kwa muktadha huu maswala makubwa haya katika serikali zetu hayapo na kama yapo sio kwa kundi kubwa kama la ndugu zangu waliopo Kule Mtimbira, Ngoilanga au Kilosa kwa Mpepo Wilaya ya Mahenge Ulanga au kule kwa watani wangu Mpapura, Naumbu au Msanga Mkuu Wilaya ya Mtwara Vijijini. Vijana wa maeneo haya wanapata taarifa hizo kwa urahisi kiasi gani na wakafaidika kwa kiasi cha kuonekana?. Imani yangu ni kuwa uwepo wa vyombo vya habari kila kona ya nchi hii ingesaidia kama sio barua maalum kutoka mamlaka za serikali basi maafisa wahusika wangekuwa angalau na kipindi redioni hasa katika vituo vya redio zilizopo huko na vijana wakapata wasaa wa kuuliza maswali na kujibiwa, mpango huu haugharimu chochote si kwa serikali au kwa afisa wa serikali. Ndio maana nasema kwa muktadha huu maswala ya UWAZI na UWAJIBIKAJI katika Serikali na Halmashauri zetu haupo. Na kwa maana hii vijana wanatumiwa tu pale wanapohitajika lakini wao wanapo hitaji hawana wa kumkimbilia. Kilio changu ni kwa vijana masikini na wasiosoma waliopo vijijini na mijini hawa serikali inawaambia nini? Hasa siku hii ya vijana duniani, Tanzania inaadhimisha kwa namna gani? Maana hili ndilo kundi kubwa na ndilo kundi litakaloleta taharuki(Political instability or social unrest) kama serikali haitaweka mikakati maalum ya kulikomboa kundi hili, tumeanza kuona mikakati ya ajira kama ajira zilivyotoka hivi karibuni au kupelekwa JKT kwa vijana ambao wamefaulu, tunashukuru sana. Lakini utaona vijana ambao hawakupata fursa ya kusoma hawapo katika mikakati hii miwili, siku hii ya Vijana serikali ingesema kitu kwa kuwa kutoa ajira kwa waliosoma na kuwapeleka JKT waliofaulu tu ni sehemu tu ya utatuzi wa kero za vijana hapa nchini na tukumbuke kuwa wasomi wanahafadhali kidogo hata wangeachwa, kuliko kuwaacha hawa ambao hawakusoma shida yake ni kubwa leo na hata siku zijazo. Tumeanza kuona kundi hili la vijana likitumika kwa migomo na vurugu mbalimbali mikoani, na naona jinsi usalama wan chi utakavyolegalega siku chache zijazo mpaka tutakapo maliza mchakato wa katiba na uchaguzi mkuu, nahakika asilimia tisini ya vijana watakaotumiwa na watu wenye nia mbaya na nchi hii ni kundi hili la vijana. Kupunguza yote haya ambayotunaona yanatokea na yanaelekea kuendelea kutokea, siku hii ya Vijana duniani ingeadhimishwa hapa Tanzania na Serikali angalau ingetutangazia au kuja na mpango wa dharula wenye lengo la kuwakwamua vijana wa Tanzania ingechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza taharuki kizi.
Maoni yangu ni kuwa Wanaharakati, wanasiasa na serikali kwa ujumla naamini kuwa sisi sote tuna mipango na mikakati ya kuwakwamua na kuwaendeleza vijana, kila mmoja wetu angetokea kuazimisha siku hii na kusema atawatendea nini vijana ili vijana walijenge taifa lao na maisha yao na familia zao.
Tumesikia katika vyombo vya habari jana(12/08/2013) Serikali ya uingereza imeshauriwa na kambi ya upinzani kuwa Makampuni yote ya kigeni na yale ya ndani kwanza yaweke kipaumbele cha ajira kwa wazawa, waziri kivuli wa Mambo ya Uhamiaji wa uingereza Mr Chrisbrant alidiliki hata kutaja majina ya kampuni zinazotoa ajira kwa wingi kwa wageni. Sisi kwetu je? Tunashindwa nini? Mbona ni swala la Kukopi na kupesti tu. BAVICHA ilibidi watamke kitu juu ya siku hii kwa namna rahisi kabisa, UVCCM hali kadhalika na Serikali pia, mashirika yasiyo ya serikali ya vijana kama TYC na mengine mengi.
Kwetu vijana tunafursa gani au tumepangiwa na kushirikishwa kupanga nini kwa maendeleo yetu? HAKUNA KITU wala HAKUNA TAARIFA YEYOTE kama ipo basi haifikiki au kueleweka kirahisi kwa kundi kubwa hili la vijana ambao hawakupata fursa ya kwenda shule na hivi sasa wamebaki wakiyumbishwa na wajanja huku serikali inaona wananchi hawa wakiteketea na madawa ya kulevya, kufungwa kutokana na ujambazi, ugaidi hata uchochezi na ushiriki wa kuvuruga amani ya nchi. Nashauri vijana tuzitumie fursa zinazojitokeza kikamilifu na tujitahidi kuto hadaika na wajanja wanaotulubuni kwa manufaa yao wenyewe. Ili amani idumu serikali hainabudi kuweka mikakati endelevu na makini sana kwa kundi hili la vijana, ni matumaini yangu kuwa wadau wote watakuwa wamepata wazo hili na kuliingiza katika mikakati na mipango yao ya maendeleo kwa mwaka unaokuja ili kuweka mambo sawa na wote tukaweza kufaidi Neema za nchi kama zilivyoletwa na mwenyezi mungu na sio wakafaidi wachache tu.
Ni mimi,
Deogratius F Makoti
a.k.a Jembe la jamuhuri
MKURUGENZI WA VOYOHEDE TANZANIA: 0714113952/0782956772
VOYOHEDE inapeda kuwapa taarifa wanaharakati vijana na vijana wote hususani wanaoishi mkoani MTWARA kuwa kutakuwa na kambi ya viana ya KITAIFA itakayofanyika jijini Dar es salaam katika kampasi ya chuo kikuu cha Dar es salaam kuanzia tarehe 29 july 2013.
Kambi hiyo inalengo la kubadilisha fikra za vijana kuhusu ajira na maisha, kambi hiyo imefadhiliwa na kuandaliwa na International Youth Fellowship(IYF) gharama za kuchangia ni Tsh 10000 tu kwa kila kijana, gharama hiyo imejumuisha mahitaji yote muhimu kama malazi, chakula na tiba ya dharula. T shirt na vipeperushi na vitabu mbalimbali pia vitagawiwa. Hakikisha hukosi katika kongamano hili muhimu, kwa wanaotoka mbali hakutakuwa na nauli, jisajili mapema nafasi ni chache. Kwa maelezo zaidi wasiliana na waratibu wa KAMBI simu namba +255 659 15 22 77. Kumbuka zimebaki siku 14 tu, "KIJANA CHANGAMKA"
Deo Makoti
MKURUGENZI.