Maswali na majibu ya wahanga wa mafuriko{Mto mzinga Mbagala Mission)
1)Mtaa wako unahitaji kitu gani?
Tunahitaji, maji safi na salama, barabara, mitaro ya kuruhusu maji kupita kwa urahisi kipindi cha mvua
2)Unaishi eneo gani? {Mtaa gani}
Mtaa wa darajani mto mzinga Mission
3}Mafuriko yameleta athari gani kwenye nyumba unayoishi na vitu vyako?
Mali zangu zote zimepotea ikiwemo ,pesa, nguo magodoro ,vitanda,na vyombo vyote vya ndani.vingine viilchukuliwa na maji wakati vilivyosalia kuchukuliwa na vibaka wakati tulipokimbia ili tusichukuliwe na maji.
mafuriko yameleta athari gani kwenye maisha yako ya kila siku?
Kupoteza mali, nyumba yagu kubomoka baadhi ya sehemu, kuvuruga mipango yangu ya kiuchumi na mipango ya maendeleo kwani sikuweza kwenda kutafuta pesa wakati nikiwa katika kipindi kigumu cha misukosuko ya mafuriko, na mtaji kupotea .Kwa ujumla nimebaki sina mwelekeo wa kimaisha.
5)Vyanzo vya ubora wa maji ,kwenu yamepata athari gani kutokana na mafuriko|?
kumekuwa na athari kubwa kwenye suala la maji kwani maji tunayotumia ni ya visima hivyo baada ya vyoo kubomoka maji tunatoyumia siyo salama kwa matumizi ya kibinadamu. Na ikizingatiwa umuhimu wa maji kwa binadamu ni uhai hivyo hatuna jinsi ya kufanya