Log in
Tanzania Women of Action(Tawa)

Tanzania Women of Action(Tawa)

Dar es salaam, Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations

Interview 7

1.Unaishi eneo gani?!

Magulumbasi 'B'

2.Mtaa wako unahitaji kitu gani sana sana?!

  • Mfereji mkubwa unaotoka barabara kubwa ya Nyerere mpaka bahari ya hindi utengenezwe ili kuruhusu maji kupita wa urahisi.
  • Kivunjwe kiwanda cha mwenye kampuni ya Ruby kilichojengwa sehemu iliyoziba mfereji wa maji.
  • Kuzibitiwe taka kwa kuwekwa sehemu maalamu ya kutupwa taka.

3.Mafuriko yameleta athari gani kwenye nyumba unayoishi na vitu vyako?!

Vitu vyangu vyote vya ndani vimechukuliwa na maji,mali zote za duka langu lililokua nyumbani lenye thamani ya zaidi ya Mil 15 kupotea.

Vifaa vyangu kama deep freezer nilivokua natumia kukopesha kwa watu kupotea.

4.Mafuriko yameleta athari gani kwenye maisha yako ya kila siku?!

  • Ajira niliyokua nategemea kutokana na duka langu haipo tena baada ya mimi kustaafu.
  • Magonjwa ya mlipuko ambayo yamemaliza akiba yangu yote iliyokua imebaki kwa gharama za matibabu kwangu na familia yangu.

5.Vyanzo vya ubora wa maji vimepata athari gani kutokana na mafuriko?!

Bomba langu limeharibika kipindi cha mvua hivyo sina njia ya kupata tena maji bila gharama ambayo sina uwezo nayo kwa sasa.

6.Kama una kazi,inakuchukua muda gani kutoka nyumbani mpaka eneo lako la kazi?!

Nimestaafu sina kazi.

January 31, 2012
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.