Fungua
Tanzania Women of Action(Tawa)

Tanzania Women of Action(Tawa)

Dar es salaam, Tanzania

 

 

Survey ya Athari za Mafuriko,Keko Wilaya ya Temeke.

Yafuatayo ni Maswali na majibu:

1.Unaishi eneo gani

Mtaa wa Magulumbasi 'A'

2.Mtaa wako Unahitaji kitu gani sana sana

Mtaa wangu unahitaji

  • Kutengenezewa mirefereji midogo midogo itayoweza kuzunguka nyumba na kupitisha maji kwa urahisi sehemu zote.
  • Kutengeneza mipaka itayosaidia kutenganisha nyumba hadi nyumba.
  • Kuhamishwa na kutafutiwa maeneo ya kuishi.

3.Mafuriko yameleta athari gani kwenye nyumba yako na vitu vyako

Vitu vyote vya ndani vilielea juu ya maji na kusombwa na kupotea,bidhaa zangu za biashara(Machinga) nazo pia zilipotea,(nguo za kike na za kiume,urembo)

4.Mafuriko yameleta athari gani kwenye maisha yako ya kila siku

Baada ya kupoteza mtaji,maisha yameendelea kuwa mabaya maana hata pesa ya kula na kutunza watoto sina.

5.Vyanzo vya ubora wa maji kwenu vimepata athari gani kutokana na mafuriko.

Maji ya kutumia kwa matumizi ya kawaida ya kisima yamechanganyika na maji taka  hivyo kuleta athari za magonjwa ya mlipuko hasa kwa watoto.

6.Kama una kazi inachukua muda gani kutoka nyumbani kwako mpaka sehemu yako ya kazi.

Kwa sasa sina kazi baada ya mtaji wangu kupotea,ila wakati bado nna ajira ilikua inanichukua dakika 15 kufika sehemu yangu ya kazi.

 

 

 

31 Januari, 2012
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Maoni (3)

Tanzania Women of Action(Tawa) (Hananasifu Kinondoni) alisema:
Janga hili ni kubwa na limeleta madhara makubwa katika maisha ya wananchi hawa,familia zimekosa mwelekeo, waathirika wakubwa ni watoto na akina mama ambao wameachwa na waume zao kwa sababu ya hali ngumu ya maisha baada ya mali zao kuteketea.Hivyo tunashauri taasisi za kimataifa .makampuni, watu binafsi kusaidia familia hizi kwani mpaka sasa serikali haijatoa msaada wowote kwa wahanga hao,
3 Februari, 2012
Tanzania Women of Action(Tawa) (Hananasifu Kinondoni) alisema:
Tungeomba vilevile suala la wanafunzi wa shule za msngi na sekondari wa maeneo tuliyotemelea waweze kupewa msaada wa haraka wa mahitaji ya shule kama yalivyoainishwa ili waendelee na masomo kwa sababu wanafunzi wengine wanaendelea na masomo ,
3 Februari, 2012
Tanzania Women of Action(Tawa) (Hananasifu Kinondoni) alisema:
Suala la afya kwa wahanga hawa wa mafuriko ni muhimu kulishughulikia kutokana na mazingira/ maeneo yao ni machafu sana na mengine bado yamezingirwa na maji ,na wahanga hawa wameshaanza kuathirika na magonjwa ya mlipuko ikiwemo maralia tukizingatia kuwepo kwa mgomo wa madakitari hii ianweza kusababisha athari kubwa ikiwemo vifo.Hivyo tunaomba misaada husika ipelekwe kwa walengwa haraka iwezekanavyo.
3 Februari, 2012

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.