Log in
SAIDIA JAMII KUISHI

SAIDIA JAMII KUISHI

Msangamkuu, Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations

BAJETI YA TANZANIA NA MATUMAINI YA WANANCHI

Nashir Pontiya (Mtwara-Tanzania)
June 17, 2011 at 4:03 PM EAT

Hivi ni kweli uchumi wa Tanzania unaendeshwa na Vileo tu? Kwani kila bajeti utaona na kusikia Sigara na Bia juu,inakuwaje hapa?

[message deleted]
Hagulwa Msusu (Dar es salaam)
June 18, 2011 at 9:10 PM EAT (edited March 26, 2012 at 8:06 AM EAT)

Hivi ukweli upo wapi?hii posho ya wabunge,ni kweli wataacha kupokea? ni kweli itatumika kwa manufaa ya umma?nikweli mjadala huu wa posho ya wabunge utafikia ukingoni kwa muafaka na manufaa ya umma?kazi kwetu wananchi.

Nashir Pontiya (Mtwara-Tanzania)
June 19, 2011 at 9:06 AM EAT (edited March 26, 2012 at 8:06 AM EAT)

Kwa jinsi ninavyoona na mikwara mingi inayowekwa na Spika wa Bunge kwa wale wote wanaokataa kupokea Posho zao ni vigumu sana wabunge wetu kuacha kupokea Posho,kwani nimegundua Wabunge wengi wametolea macho sana hizo Posho,Lakini hata muda mwingine najiuliza kitu kimoja hivi hata hizi Posho wabunge wetu wakiziacha hivi ni kweli zitapelekwa kwa mafungu ya maendeleo ya Halmashauri na hata zikipelekwa huko zitafanyakazi zilizokusudiwa?

itony (Dar es salaam)
June 19, 2011 at 1:47 PM EAT (edited March 26, 2012 at 8:06 AM EAT)

kwa kweli hili ni tatizo kubwa sana. Hizi posho sio kwamba jamaa hawazitaki kweli ila wanajaribu kufikisha ujumbe kwamba wanapo panga kiasi cha hizi posho, basi waangalie na kiasi ambacho huenda kwenye mifuko ya maendeleo. Sio mfuko wa maendeleo una bilioni moja lakini posho bilioni 900


Add New Message

Invite people to participate