Tanzania kuwa mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa kuhusu uhifadhi wa mbuga za wanyamapori
Wizara ya Maliasili na Utalii inatoa taarifa kuwa Tanzania itakuwa mwenyeji wa Kongamano la Kwanza la Africa kuhusu Uendeshaji, Changamoto na Fursa za Uhifadhi wa Mbuga za Wanyamapori na Meneo yaliyohifadhiwa. Ifuatayo ni taarifa kamili kwa umma.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
TAARIFA KWA UMMA
TANZANIA KUWA MWENYEJI WA KONGAMANO LA KIMATAIFA KUHUSU UHIFADHI WA MBUGA ZA WANYAMAPORI
Wizara ya Maliasili na Utalii inatoa taarifa kuwa Tanzania itakuwa mwenyeji wa Kongamano la Kwanza la Africa kuhusu Uendeshaji, Changamoto na Fursa za Uhifadhi wa Mbuga za Wanyamapori na Meneo yaliyohifadhiwa (The 1st Pan-African Conference on Sustainable Tourism Management In National Parks and Protected Areas: Challenges and Opportunities). Kongamano hilo limepangwa kufanyika katika kituo ya cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 15 hadi 19 Oktoba 2012. Washiriki wapatao 300 kutoka nchi mbalimbali wanatarajia kuhudhuria mkutano huo.
Tanzania imeteuliwa kuwa mwenyeji wa Kongamano hilo na Shirika la Umoja wa Mataifa Utalii Duniani (UNWTO) kufuatia mkutano wake (UNWTO General Assembly) ambao ulifanyika nchini Korea tarehe 14 hadi 18 Oktoba 2011. Katika Mkutano huo Tanzania ilichaguliwa kuwa mjumbe katika Baraza la Utendaji (Executive Council) la Shirika hilo hadi mwaka 2015. UNWTO ni shirika la Umoja wa Mataifa linaloongoza masuala ya Sera, Mafunzo, Uendelezaji na Utangazaji katika sekta ya utalii duniani.
Kongamano hilo la Oktoba 2012 ambalo ni la kwanza la aina yake litawakuwakutanisha wahifadhi na wadau wa sekta ya Utalii ili wajadili namna ya kufanikisha uhifadhi na utalii. Tanzania imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa Kongamano hilo kutokanana na sifa nzuri na uzoefu tulio nao katika kuanzisha na kuendesha hifadhi za Taifa.
Tanzania itanufaika kwani washiriki wa Kongamano hilo watapata fursa ya kutembelea vivutio vyetu vya utalii, watatumia fedha kwa malazi, chakula, burudani na huduma nyingine watakazotumia wakiwa hapa nchini na hivyo kuacha fedha katika mzunguko wa kiuchumi hapa nchini. Aidha, tutatumia Kongamano hilo kutangaza vivutio vyetu vya utalii. Faida nyingine kubwa ni kuwa, washiriki wa Tanzania watapata fursa kushiriki kwenye Kongamano hilo kwa gharama nafuu na watapata nafasi ya kubadilishana ujuzi na ueledi kutoka kwa wenzao wa nchi za nje.
Wito unatolewa kwa wanachi, wafanyabiashara na wadau wote kujiandaa ipasavyo ili kunufaika na ujio huo wa kimataifa. Taarifa mbalimbali zitaendelea kutolewa kuhusu maendeleo ya matayarisho ya mkutano huo
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
16 Februari 2012
Promise to market Tanzania tourism in the Middle East
H.E. Ambassador Mohammed Hamza (left) shakes hands with the Managing Director of Tanzania Tourist Board
Dr. Aloyce Nzuki (Right).
The newly appointed Tanzania Ambassador to Egypt, H. E. Mohammed Hamza, has pledged to promote the country’s tourism potential in the Middle East market.
The promise was made recently during a courtesy call on the Tanzania Tourist Board (TTB) Managing Director, Dr. Aloyce Nzuki, in Dar es Salaam, where the Ambassador also pledged to attract Egyptian businessmen to invest in tourism industry and interest Egypt Air to increase flight frequencies to the country.
To that effect, the Ambassador called on TTB to collaborate with the Embassy in organizing educational trips for Egyptian tour operators, investors and journalists to Tanzania in order to tap more into the Middle East market.
The Ambassador noted that it is now high time Tanzania vigorously market itself in the Middle East as it is a market targeted by many other destinations worldwide.
Regarding cultural and historical products, Ambassador Hamza concurred with Dr. Nzuki’s request for assistance in getting some experts from Egypt who can help and impart knowledge on how to conserve and restore ancient ruins and historical sites including those in Bagamoyo, Kilwa and Zanzibar, because Egypt is famous for its historical sites and monuments.
The Managing Director also requested the Ambassador to arrange for the translation of TTB website into Arabic and secure opportunities for the TTB staff and others from the private sector to learn Arabic language in order to effectively tap into the market.