Envaya

 

LISHE DUNI, AFYA DHAIFU NA UMASKINI

Ingawa Tanzania imepiga hatua katika nyanja mbalimbali za afya, bado hali ya lishe si nzuri. 42% ya watoto wa Tanzania walio chini ya umri wa miaka mitano wanakabiliwa na udumavu, hii ni hali mbaya kwa mjibu wa Shirika la Afya Dunian (WHO) ambalo linautazama udumavu katika nchi kuwa ni wakutisha pale unapozidi 40%.1/3 ya watoto wenye umri kati ya miezi 6 na 59 wana upungufu wa madini chuma na vitamini A. Takribani 1/3 ya wasichana na wanawake wenye umri kati ya miaka 15 na 49 wana upungufu wa madini ya chuma, madini joto na vitamini A na 2/5 wana upungufu wa damu na 1/10 ya wanawake wana lishe duni kwa ujumla.

Hali duni ya lishe katika Tanzania, huchangia kutokea kwa vifo 130 vya watoto kila siku. Chanzo cha vifo ni upungufu wa kinga ya mwili ya kujikinga na magonjwa mbalimbali kwa sababu ya lishe duni. Watoto wanaonusurika kifo, hukabiliwa na uduni wa akili na kushindwa kumudu masomo shuleni. Uwezo wa kiakili hushuka kwa kiwango cha 13.5 IQ na watu wazima wenye lishe duni hushindwa kufikiri sawasawa na hawawezi kufanya kazi kwa ufanisi. Hali hii huongeza tatizo la umaskini nchini.

Ingawa tatizo linaweza kuwa upatikanaji wa chakula cha kutosha, bado mikoa yenye chakula cha kutosha kama Iringa, Mbeya na Rukwa inakabiliwa na tatizo la lishe duni miongoni mwa jamii. Hii inaonyesha kuwa kuna tatizo la kutokuelewa jinsi ya kutumia vyakula kwa manufaa au kutokujua vipaumbele vya maisha.Wakati hayo yote yakitokea, wanawake wengi hununua nywele bandia na vipodozi vya gharama vinavyo dhuru afya na akina baba hutumia pesa katika ulevi, anasa na kununua vyakula visivyokuwa na lishe kama vile vinywaji baridi vya viwandani.

Lishe duni ni tatizo linalozuilika na kwa kutambua hivyo sisi (MANSHEP) tumeamua kuunga mkono jitihada za serikali za kupambana na tatizo hili. Pia tunaunga mkono jitihada za wadau wengine kama vile Global Alliance for Improved Nutrition (GAIN), www.gainhealth.org na Flour Fortification Initiative(FFI), www.ffinetwork.org katika kuboresha lishe ya jamii.

Tunatoa mafunzo ya kuandaa unga wa lishe na huduma ya kusambaza unga wa lishe kwa ajili ya lishe ya jamii. Tushirikiane, Tanzania bila lishe duni inawezekana

Chanzo: UNICEF-Nutrition Overview(www.unicef.org/10787_11047. htm).

 

January 1, 2014
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.