Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

Kule dodoma hasa  vijijini wanahitaji msaada  twendeni  tukatoe elimu kumbuka elimu ni mtaji mkubwa kuliko mabilioni ya fedha karibuni wadau wa maendeleo na wakeleketwa wa maendeleo.

April 21, 2017
« Previous Next »

Comments (3)

ALLIANCE FOR SOCIAL CHANGE (KILINDI TANGA TANZANIA) said:
Ukitaka kumsaidia mtu mboga mpe ndoano sio samaki, Tutoeni elimu ni ndoano na samaki ni fedha, au chakula. karibuni sana.
April 21, 2017
ALLIANCE FOR SOCIAL CHANGE (KILINDI TANGA TANZANIA) said:
Madawa ya asili ni mengi ila bado hajafanyiwa utafiti wa kutosha kuhusu aina ya wadudu na magonjwa ninayotibu, jinsi ya kutumia na kiasi cha kutumia. Baadhi ya mimiea inayotoa madawa ya asili ni mbegu na majani ya muarobaini, tumbaku, pilipili kali, pareto, kitunguu swaumu, manung'anung'a, n.k. Muarobaini ni miongoni mwa mimea michahce ambayo mpaka sasa imefanyiwa utafiti wa kiina. Mfano, kuchanganya nusu kilo ya mbegu za muarobaini zilizotwangwa katika lita ishirini za maji husaidia kuua wadudu mbalimbali wakiwemo funza wanaotoboa matunda ya nyanya.

Madawa ya asili ni bora zaidi kuliko madawa ya viwandani kwani sumu yake ni kidogo na hupungua haraka baada ya kupiga dawa. Hivyo ni salama zaidi kwa mpigaji dawa na mlaji mboga. Hivyo kupendekezwa katika kilimo hai na hifadhi ya mazingira.

Kasoro kubwa katika kutumia madawa ya asili ni kwamba hayajafanyiwa utafiti wa kutosha ukilinganisha na yale ya viwandani. Mfano, nitumie dawa ipi inayofaa kwa mdudu yupi?. Nguvu yake ni kidogo, hayatafaa kuzuia mashambulizi makubwa ya magonjwa au wadudu vilevile yanakinga zaidi mboga dhidi ya wadudu waharibifu kuliko magonjwa.Pia uwiano wa kuchanganya dawa na maji bado haujulikani vizuri. Mfano, niweke kiasi gani cha dawa katika kiasi gani cha maji ?..
April 21, 2017
ALLIANCE FOR SOCIAL CHANGE (KILINDI TANGA TANZANIA) said:
Tunaweza kubadili mwanga wa jua moja kwa moja kuwa umeme kwa kutumia seli ya jua.

Mwanga wa jua unapopiga Paneli za Jua kwa chembe za miali yake zinazojulikana kama fotoni (Kwa kiingereza photons),panaeli za jua hubadili fotoni hizo kuwa electroni zinazofanya mkondo mnyoofu wa umeme-aina hii ya umeme inaitwa Umeme Jua.

Electroni hizi hutoka katika paneli na kuingia katika kifaa kiitwacho Inveta ambacho huubadili kuwa mkondo geu wa umeme.

Huu ni umeme ambao hutumika na vifaa vingi vya majumbani kama pasi,taa ,redio na TV.
Seli za Jua

Seli za nishati ya jua zinaundwa na paneli za umbo mraba zilizotengenezwa na madini ya silikoni na mengine yenye kupitisha umeme.

Mwanga wa jua unapopiga seli hizi,athari za kikemikali husababisha elektoni kutoka na kuzakisha mkondo wa umeme.

Seli hizi zinaitwa kitaalamu “Photovoltaic Cells” au “PV Cells” ambazo hutumika pia katika vifaa kama mashine za hesabu,saa au kompyuta ndogo.

umeme-jua_seli
April 21, 2017

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.